Matangazo ya kibiashara
Kwenye pwani ya Cabo Delgado kuna uwanja mkubwa zaidi wa gesi unaofahamika kote duniani. Shughuli za uchimbaji wake, zinazotekelezwa na kampuni ya Ufaransa Total, inayoongoza muungano wa kimataifa, zilianza tena mnamo mwezi Januari baada ya kusimamishwa kwa miaka kadhaa kwa sababu za usalama.
Kuanza tena kwa shughuli hizi kumeongeza matumaini makubwa miongoni mwa jamii za wenyeji, huku migogoro mingi ikiwa bado haijatatuliwa. Kipindi cha pili cha uchunguzi wa “Mozambique Exposed” uliofanywa na muungano unaoratibiwa na Forbidden Stories, ambapo RFI ilichangia.
Katika sebule ya abiria wanaoondoka katika uwanja wa ndege wa Pemba, mwanzoni mwa mwezi Mei, abiria wapatao kumi wananong’oneza kati yao. Ni saa moja asubuhi, na baadhi wanajaribu kupata usingizi wao mfupi wa usiku. Wasafiri ni wafanyakazi wa misaada ya kibinadamu wakisubiri ndege yao iliyokodishwa na Umoja wa Mataifa kwenda Mueda, Mocimboa da Praia, au Palma, kilomita mia chache kutoka Pemba.
Ghafla, wanaume wanne wenye misuli wanasimama. Rubani anawavaa jaketi za kuokoa maisha za ajabu, tambarare, na zenye rangi nyingi. Kundi hilo linapanda kwenye lami ya uwanja wa ndege na kupanda helikopta. “Wao wanaenda mjini Afungi,” anasema mmoja wa wafanyakazi hao wa misaada ya binadamu. “Wanatua moja kwa moja kwenye kambi ya Kampuni ya Total.”
Mfumo Uliofungwa
Afungi ni Peninsula ao rasi iliyo karibu na jiji la Palma kaskazini mwa Msumbiji, umbali mfupi kutoka Tanzania. Hapo ndipo kanpuni ya Total na washirika wake wameanzisha eneo la mradi wao wa uchimbaji gesi ya LNG ya Msumbiji: uchimbaji wa shamba la pwani katika Bonde la Ruvuma na ujenzi wa kituo cha kuyeyusha Gesi ya methane eneo la pwani.
Akiba hiyo inakadiriwa kuwa mita za ujazo bilioni 5. Hizi ndizo kubwa zaidi duniani. Kwa mradi huu mkubwa, wa kampuni ya Total inaungwa mkono na washirika kadhaa wa kimataifa, ikiwa ni pamoja na makampuni matatu ya mafuta ya India, kampuni ya Kijapani Mitsui, na jimbo la Msumbiji, ambalo lina hisa ya asilimia kumi na tano 15%.
Kituo cha Afungi kina ukubwa wa hekta 7,000 za ardhi yenye kuzungukwa na uzio. Katikati yake kuna uwanja wa ndege wenye lami , iliyozungukwa na makazi ya wafanyakazi na mtandao wa maghala. “Makampuni ya kigeni huwatenga wafanyakazi wao. Hii haileti faida yoyote kwa maendeleo ya ndani,” analalamika Abudo Gafuro, mwanaharakati wa shirika la haki za binadamu Kundeleya.
Tangu mwaka wa 2017, Cabo Delgado imekuwa ikikumbwa na vurugu kutoka kwa kundi la Kiislamu lenye silaha. Kundi la Al-Shabaab ambalo linadai kuanzisha Sharia na utaratibu mpya wa kijamii ambao ungeruhusu usambazaji wa utajiri kwa haki zaidi huko Cabo Delgado.
Kulingana na shirika lisilo la kiserikali la ACLED, mzozo huo tayari umesababisha vifo vya zaidi ya watu 6,500, na Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa angalau watu 800,000 walilazimika kukimbia makazi yao.
Mwaka 2020, Kampuni ya Total iliamua kusimamisha mradi wa LNG wa Msumbiji. Na kuuanzisha tena mwezi Januari mwaka huu.
Kuhama, Fidia, na Kukatishwa Tamaa
Akiwa ameketi kwenye kiti kwenye kivuli cha mti wa mshita, José Cheila [jina limebadilishwa] amechoka. Siku chache mapema, alihudhuria mkutano wa jamii kuhusu masuala ya ardhi. “Mwakilishi wa Total hakuonekana hata,” analalamika mratibu huyu wa asasi za kiraia kutoka Palma. Kwa karibu miaka kumi, suala la fidia kutokana na unyang’anyi wa ardhi ya mamia ya wakulima na wavuvi katika eneo hilo halijatatuliwa.
Nchini Msumbiji, ardhi inamilikiwa na serikali, ambayo hata hivyo na yenyewe inatambua matumizi ya pamoja, ya mtu binafsi, na ya kitamaduni ya jamii hizo.
Mnamo mwaka wa 2012, mamlaka ya Msumbiji ilitoa haki ya matumizi na unyonyaji wa ardhi (maarufu kama DUAT) kwa kampuni ya mafuta ya Anadarko yenye makao yake Texas, ambayo iligundua uwanja wa mafuta wa Ruvuma. Ilikuwa DUAT hii (Kitengo cha Maendeleo ya Eneo hilo) ambayo Kampuni ya Total na washirika wake waliirithi walipochukua mradi huo mnamo 2019.
Inatoa makazi mapya kwa wakazi, fidia ya kifedha ya mtu binafsi na ya pamoja, pia michango ya vifaa kama vile pikipiki. José Cheila anaona fidia hii kuwa ya haki, lakini bado haijatimia.
“Karibu meticais milioni 184 [karibu sawa na yuro milioni 2.5] kama fidia ilipangwa mwaka wa 2014, lakini familia bado zinasubiri kwa sababu mradi huo ulisimamishwa,” anasema Eduardo Caponde wa Kituo cha Maendeleo ya Jamii cha Cabo Delgado, akiwa mwenye kukosa subira.
Kwa kuanza tena kwa mradi wa LNG wa Msumbiji, matarajio ya jamii ni makubwa. “Majadiliano yameanza tena,” ameongeza Eduardo Caponde, “lakini maswali mapya yanaibuka: je, kiasi kilichoamliwa mwaka wa 2014 bado ni halali kwa leo? Hasa kwa kuwa gharama ya maisha huko Palma imebadilika na kuwa ngumu.”
“Katika mawasiliano na muungano wetu, Kampuni ya Total imehakikisha kwamba familia zote 643 zilizoathiriwa na mradi wa LNG wa Msumbiji zimehamishiwa kwenye kijiji cha Quitunda. “Mwishoni mwa 2025, shughuli za kulipa fidia ya ardhi zilizoainishwa katika mpango wa makazi mapya zote zilikamilika,” Kampuni ya Total iliandika majibu yake katika barua pepe. Kampuni kubwa ya mafuta na gesi ya Ufaransa pia inadai kwamba “programu za kurejesha riziki” zimetekelezwa.
Bunker
Chanzo kingine kinachokatisha tamaa ni kutengwa kwa mradi huu wa LNG wa Msumbiji, ambao haufanikishi jamii za wenyeji kupata faida. Mnamo Septemba 2025, Kampuni ya Total ilisaini mkataba na Shirika la Maendeleo Jumuishi la Kaskazini.
Kwa bajeti ya yuro milioni nane nukta tano, €8.5, mpango huu unakusudiwa kufadhili miradi ya kazi na pia mapato yote katika wilaya za Palma na Mocimboa da Praia.
Lakini hii haijawashawishi wakazi wa eneo hilo. “Jamii zilitarajia kwamba wafanyakazi wanaohusika na uchimbaji wa gesi wangeenda kwenye migahawa na hoteli, pia kutumia teksi za pikipiki,” anaeleza Aly Caetano, mratibu wa Kituo cha Maendeleo na Haki za Binadamu (CDD) huko Cabo Delgado. Baadhi ya wajasiriamali wameingia kwenye deni la kuweka dau kwenye shughuli hii ya maendeleo.
Lakini hawawaoni kamwe watu kutoka Kampuni ya Total.Suala lingine ambalo limeongezwa kwa hili ni suala la usalama mdogo uliokithiri unaozunguka eneo hilo la uchimbaji wa gesi, huku wakazi wa eneo hilo wakipata mashambulizi ya mara kwa mara yanayotekelezwa na kundi lenye silaha la al-Shabaab.
Tishio kwa Haki za Binadamu
Mnamo Machi 24, 2021, jiji la Palma lilishuhudia shambulio baya zaidi katika historia yake. Mamia ya wapiganaji wa kundi hilo walipora, wakaua, na kudhibiti jiji kwa karibu wiki mbili. Idadi ya vifo inakadiriwa kuwa takriban watu 1,500.
Kwa mujibu wa tarifa kutoka kwa wakazi, mamia kadhaa kati yao walifanikiwa kufika kwenye península ama rasi ya Afungi. Mradi wa uchimbaji wa gesi ulisitishwa wakati huo, na wafanyakazi wachache ndio walikuwepo. Hata hivyo, uhamisho wa watu ulipangwa kwa kutumia boti hadi Pemba.
Wale waliobaki waliteseka sana kwa ukatili wa kulipiza kisasi na Vikosi vyenye Silaha vya Msumbiji (FADM) walipouteka mji huo tena. “Ni wanajeshi wetu waliokuwa wakituua ambao ni Ndugu zetu,” anasema José Cheila.
Kesi mbili zimefunguliwa dhidi ya Kampuni ya Total kuhusiana na shambulio la Palma. Ya kwanza, ambayo ilisikilizwa mnamo mwaka wa 2023, ilifunguliwa katika mahakama ya Nanterre na manusura watatu pia wanufaika wanne wa waathiriwa, wenye uraia wa Uingereza na Afrika Kusini.
Wakilishutumu jitu hilo la Ufaransa kwa mauaji bila kukusudia na kushindwa kumsaidia mtu aliye hatarini, kutokana na “uzembe” wake katika kusimamia usalama wa wafanyakazi wake na wakandarasi wadogo.
Mnamo mwaka wa 2025, malalamiko mengine yaliwasilishwa katika Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Kitaifa wa Kupambana na Ugaidi (PNAT) na Kituo cha Ulaya cha Haki za Kikatiba na Binadamu (ECCHR) kwa kosa la kushiriki katika uhalifu wa kivita, mateso, na kutoweka kwa watu kwa lazima. Shirika lisilo la kiserikali la Ujerumani linachunguza uhusiano kati ya Total na FADM (Vikosi vya Jeshi la Msumbiji), ambavyo vina jukumu la kulinda, miongoni mwa mambo mengine, tovuti ya LNG ya Msumbiji.
Mkataba wa Maelewano
Mnamo mwaka wa 2020, mradi wa LNG wa Msumbiji ulisaini mkataba wa maelewano na serikali ya Msumbiji. Mkataba huo Unatoa nafasi kwa wafanyakazi wa FADM (yaani Vikosi vya Wanajeshi vya Msumbiji) ndani na karibu na rasi ya Afungi. Hiki ni Kikosi Kazi cha Pamoja (JTF), kinachoundwa na takriban wanajeshi 600 wa Msumbiji, ambapo asilimia kumi 10% kati yao ni “fusileros,” wanajeshi wasomi waliofunzwa na Marekani.
Makubaliano hayo yanaeleza kwamba mradi wa uchimbaji wa gesi utafadhili chumba cha wanajeshi na chakula. Bonasi pia hulipwa kwa wanajeshi, kulingana na cheo chao. Ukiukwaji wa haki za binadamu au ukiukwaji husababisha kuondolewa moja kwa moja kwa bonasi hii.
Kulingana na ripoti ya ukaguzi wa ndani ya 2023 iliyoagizwa na Total na kufanywa kwa sehemu na mwanadiplomasia wa zamani wa kibinadamu na mwanadiplomasia wa Ufaransa Jean-Christophe Ruffin, hali hizi nzuri zilitolewa na kundi hilo ili kulinda FADM kutokana na kishawishi cha kutumia vibaya madaraka yao, kwani hali duni ya maisha ya vikosi vya wanajeshi vya Msumbiji inajulikana sana.
Hata hivyo, ripoti hiyo inaibua swali lifuatalo: “Kuwepo kwa uhusiano wa kifedha wa mtu binafsi na wanajeshi wa JTF kumeunda uhusiano wa moja kwa moja kati ya LNG ya Msumbiji na wanajeshi hawa. Ni pasina shaka kwamba bonasi hii ya ‘masharti’ ingewea kuwa na athari ya kuzuia ukiukwaji unaowezekana.
Katika tukio la ukiukwaji wa haki za binadamu, suala hili linahusisha moja kwa moja jukumu la muungano.” Mnamo mwaka wa 2021, bonasi iliyolipwa kwa JTF na mradi wa LNG ya Msumbiji ilisitishwa kufuatia madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanywa na jamii za wenyeji. Hizi zilikuwa “ukiukwaji dhidi ya wavuvi wawili,” Total inabainisha, bila uhusiano na vurugu zilizofanywa wakati wa ukombozi wa Palma.
Kwa upande wao, mamlaka ya Msumbiji hawajawahi kufungua uchunguzi kuhusu matukio huko Palma.