Mahakama ya Tunisia imewaachilia kundi la wafanyakazi wa misaada baada ya kuwapa vifungo vya nje kwa kosa la kuwezesha ‘kuingia na kukaa bila vibali’ kwa wahamiaji, ilisema kamati ya msaada siku ya Jumanne.

Sherifa Riahi, mkurugenzi wa zamani wa Shirika lisilokuwa la serikali la Terre d’Asile, na baadhi ya wafanyakazi wake walikuwa tayari wamekaa gerezani kwa zaidi ya miezi 20 kabla ya kusikilizwa kwa kesi yao Jumatatu.

Saa chache baada ya kusikilizwa, kamati ya msaada ya Riahi ilitoa video ikimuonyesha akiondoka gerezani usiku na kutangaza kuwa wenzake pia wameachiliwa.

Mahmoud Daoud Yaacoub, mmoja wa mawakili wa upande wa utetezi wa Riahi, aliiwaambia waandishi kuwa mahakama ilitoa hukumu hiyo ya kusimamishwa kwa miaka miwili kwa watuhumiwa waliokuwepo kizuizini kabla ya kesi.

Mashtaka mengine yalifutwa

“Kesho tutaelewa hukumu iliyosalia kuhusu watuhumiwa waliotolewa kwa dhamana,” alisema.

Wafanyakazi wa NGO walituhumiwa pamoja na wafanyakazi wengine 17 wa manispaa kutoka mji wa mashariki wa Sousse ambao walihusishwa kwa kukodisha majengo kwa shirika.

Watuhumiwa 23, ambao pia walishtakiwa kwa ‘kufanya njama kwa lengo la kuwahifadhi au kuwaficha watu walioingia kwa njia haramu nchini’, walikabiliwa na adhabu ya hadi miaka 10 gerezani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *