Sasa Baraza hilo limetoa wito kwa vyombo vya dola na maafisa wa afya kusaidia kuwalinda wananchi dhidi ya taarifa potofu za kiafya na kuhimiza ushirikiano wa karibu kati ya viongozi wa dini na wataalam wa matibabu ili kulinda afya ya umma.

Upande wa serikali, kulikuwa na kauli kali zaidi ambapo Waziri wa Afya Aden Duale alitaka uchunguzi kuanzishwa dhidi ya mhubiri huyo na ikiwezekana afunguliwe mashtaka.

Wakenya mtandaoni wamekuwa na kauli za kutofautiana huku baadhi wakiunga mkono amri ya kukamatwa na kushtakiwa kwa Owuor na wenzake. Lakini wapo wanaomtetea na kusema kuwa Owuor kwamba anao uwezo wa kuwaponya wagonjwa.

Haya yanawakumbusha Wakenya matukio ya 2023 ya Shakahola, ambapo zaidi ya watu 400 walifariki kutokana na kumfuata mhubiri wa kanisa la Good News International, Paul Mackenzie, aliyewaagiza kufunga kula na kunywa ili waende kukutana na Yesu Kristu.

Owuor alianzaia wapi?

Mhubiri huyo alikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya mauaji, ugaidi, utesaji watoto na mauaji bila kukusudia. Kesi yake bado inaendelea.

Mhubiri Owuor anaongoza kanisa la Repentance and Holiness. Anaaminiwa kumiliki shahada ya uzamivu katika biokemia na alifanya kazi kama mhadhiri wa chuo nchini Marekani kabla ya kurudi Kenya mwaka 2000 na kuanzisha kanisa lake.

Owuor, mbali na madai yake ya kutibu kwa kutumia miujiza, lakini pia amezua mjadala mkubwa kutokana na madai yake ya kuwa na uwezo wa kutabiri majanga makubwa ya dunia kabla hayajatokea.

Pia ni miongoni mwa wahubiri matajiri zaidi nchini Kenya akidaiwa kumiliki magari ya kifahari, ndege za binafsi na majumba makubwa ya yakifahari, huku akionekana katikati ya walinzi akiwa katika msafara mrefu kila anapokwenda.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *