
Serikali ya taifa hilo haikuwa imetoa idadi ya waliouawa hapo awali, lakini jeshi lilichapisha orodha ya majina 23 ya wanajeshi wake waliokufa. Maafisa wa Venezuela wamesema sehemu kubwa ya kikosi cha ulinzi cha Maduro kiliuawa “kwa kikatili,” na Cuba imesema wanajeshi na maafisa wake wa kijasusi 32 waliokuwa Venezuela waliuawa, Mke wa Maduro, Cilia Flores, aliyekamatwa pamoja naye, alipata jeraha la kichwa wakati wa uvamizi wa Marekani na Maduro alipata jeraha kwenye mguu wake. Jumanne iliyopita Rais wa mpito wa Venezuela, Delcy Rodriguez alitangaza wiki moja ya maombolezo kwa wanajeshi waliouawa katika uvamizi huo.