
Denmark inabaini “fursa imefunguliwa” kwa “mazungumzo ya kweli” na Marekani kuhusu usalama huko Greenland. Waziri Mkuu Mette Frederiksen pia amesema kwamba nchi zote za NATO zinakubaliana kuhusu “uwepo wa kudumu” wa NATO katika Aktiki.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Nchi zote za NATO zinakubaliana kuhusu uwepo wa kudumu wa Muungano katika Aktiki na karibu na Greenland“, Waziri Mkuu wa Denmark Mette Frederiksen amebainisha siku ya Alhamisi. “Kila mtu ndani ya NATO anakubaliana kuhusu jambo hili…: tunahitaji uwepo wa kudumu wa NATO katika eneo la Aktiki, ikiwa ni pamoja na karibu na Greenland,” alitangaza alipowasili Brussels kwa mkutano wa viongozi wa Umoja wa Ulaya, EU.
Denmark inaona fursa ya kujadiliana na Marekani kuhusu masharti ya usalama ulioimarishwa huko Greenland, kufuatia tangazo la mkataba wa makubaliano kati ya Donald Trump na Katibu Mkuu wa NATO, Waziri wa Mambo ya Nje Lars Løkke Rasmussen alisema siku ya Alhamisi.
Fursa imefunguliwa kwetu kwa mara nyingine tena kuwa na mazungumzo ya kweli kati ya Denmark na Greenland kwa upande mmoja—na Marekani kwa upande mwingine,” waziri huyo alisema katika mkutano wa pamoja na waandishi wa habari na mwenzake wa Sweden, Maria Malmer Stenergard.
“Kwa hivyo nadhani tunashiriki malengo, lakini sio lazima mbinu, lakini hii sasa inafungua uwezekano wa kuweka mambo mahali pake,” aliongeza.
Waziri Mkuu wa Greenland alitoa wito wa “mazungumzo ya amani” kuhusu mustakabali wa kisiwa hicho, huku akisisitiza kwamba uhuru ni “mstari mwekundu.” Jens-Frederik Nielsen pia alisema hajui makubaliano yaliyotajwa na Donald Trump yana nini ndani yake.