Nchini Burkina Faso, Chama cha Wanasheria kinashutumu kukamatwa kwa wakili Ini Benjamine Doli. Aliporejea kutoka likizo nje ya nchi, “alitekwa nyara” kutoka nyumbani kwake huko Ouagadougou na watu wenye silaha.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Ini Benjamine Doli albaye ni mkosoaji mkubwa wa utawala wa kijeshi, hivi karibuni alituma barua ya wazi kwa Rais wa Urusi Vladimir Putin, akimtaka kuingilia kati na kuwashawishi “viongozi” wa Muungano wa Nchi za Sahel, ili waache kuchafua “taswira” na “heshima” ya Urusi kwa kuihusisha na vitendo vya uhalifu.

Habari za “kutekwa nyara” kwa wakili huyo na watu wenye silaha usiku wa Agosti 31 kuamkia Septemba 1 zilienea kwenye mitandao ya kijamii. Kulingana na Chama cha Wanasheria wa Burkina Faso, “watu wenye silaha waliojitambulisha kama askari, waliingia kwa nguvu nyumbani kwa wakili huyo na kumchukua kwa nguvu, wakichukua vifaa vyake na kompyuta.”

Iliwachukua mawakili hao siku kadhaa kuthibitisha kwamba yuko chini ya mikononi mwa mwa mahakama. Vitendo ambavyo hutokea mara kwa mara, ambavyo “havihusiana na utaratibu wa sheria za uhalifu,” kulingana na mawakili hao, ambao wanadai kuachiliwa kwake mara moja na kuheshimiwa kwa sheria.

Kinachomponza Blaise Bazié: jioni ya Septemba 6, mwendesha mashtaka katika Mahakama Kuu ya Ouagadougou alisema kuwa uchunguzi umefunguliwa kwa “uhaini, kumtusi mkuu wa nchi, na kujaribu kuwavunja moyo wanajeshi.” Bw. Doli ambaye ni mkosoaji mkubwa wa serikali, hivi majuzi aliandika kwamba “jeshi la Burkina Faso halijawahi kuwa na taswira mbaya kama linavyofanya sasa.”

Alikuwa akihoji “jinsi gani raia, mashahidi wa utekaji nyara, mateso, na unyanyasaji” unaofanywa na serikali, wangeweza kushirikiana na jeshi. Hata aliandika barua ya wazi kwa rais wa Urusi akimtaka awahutubie viongozi wa Muungano wa Nchi za Sahel kuhusu tabia zao mabaya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *