Mashambulizi ya makombora siku ya Jumatano yaliwaua watu 12 zaidi.

Hospitali nyingi mjini Al-Fasher zimeshambuliwa kwa mabomu kila mara na kulazimika kufungwa, kuacha karibu asilimia 80 ya watu wa mji huo wakihitaji huduma ya afya lakini hawana njia ya kufikia huduma hiyo, kulingana na Umoja wa Mataifa.

Kote nchini, hospitali zimekuwa zikishambuliwa mara kwa mara, kuvamiwa na wapiganaji na kuporwa, huku chama cha madaktari kikisema kuwa asilimia 90 ya hospitali kwa wakati fulani zimelazimika kufungwa.

Wahudumu kadhaa wa afya wameripotiwa kuuawa, ikiwemo kile ambacho Umoja wa Mataifa kinasema mashambulizi yaliyowalenga kwa makusudi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *