Watu wenye silaha wamevamia Jumba la Makumbusho la Louvre siku ya Jumapili asubuhi, Oktoba 19, katika ufunguzi wa Makumbusho ya Louvre, wakati ambapo vito vya “thamani ya bei nafuu” viliibiwa, kulingana na Waziri wa Mambo ya Ndani Laurent Nuñez. Hivi ndivyo inavyojulikana kuhusu wizi huu.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Majambazi waliojihami kwa silaha wameiba vito vilivyoonyeshwa kwenye Jumba la Makumbusho la Louvre mjini Paris siku ya Jumapili asubuhi kabla ya kutimka. Kulingana na uchunguzi wa awali, tukio hilo lilitokea kati ya 3:30 asubuhi na 3:40 saa za ndani. Jumba la makumbusho lilikuwa limefungua milango yake saa 3:00 asubuhi.

Wezi hao walivamia eneo la Matunzi la Apollo la jumba hilo la makumbusho, linalohifadhi Vito vya Taji vya Ufaransa, na kuvunja madirisha ya chumba hicho kwa mashine za kukata vyumba baada ya kupanda kwenye chuma kwa kuingia katika jumba hilo. Vito hivyo vilikuwa vinalindwa na vio viwili vya ulinzi wa hali ya juu.

Kulingana na Waziri wa Mambo ya Ndani Laurent Nuñez, operesheni hiyo ilidumu “dakika saba tu.” Amesema ana “matumaini” kwamba wahalifu, ambao walikimbia kwa skuta, watakamatwa “haraka sana.”

Ni vitu gani viliibiwa?

Siku ya Jumapili jioni, Wizara ya Utamaduni imetangaza katika taarifa kwa vyombo vya habari kwamba vito vinane “vya thamani ya urithi isiyoweza kukadiriwa” vimeibiwa kutoka Louvre. Hapo awali, Laurent Nuñez aliviambia vituo vya France Inter, France Télévision, na Le Monde kwamba wahalifu waliiba “vito ambavyo vina thamani halisi ya urithi.” Nyumba ya sanaa ya Apollo ambayo ilijengwa kwa ombi la Louis XIV,  ina mkusanyiko wa kifalme wa vito na Almasi za Taji, ikijumuisha vipande vitatu vya kihistoria: Regent, Sancy, na Hortensia.

Wakati wa kukimbia kwao, wahalifu waliacha moja ya vito, ambayo ilipatikana “karibu na Louvre,” Waziri wa Utamaduni Rachida Dati alitangaza saa sita mchana. Ni taji malkia Eugenie, mke wa Napoleon III. taji hiyo, mfano wa uwakilishi wa taji za kifalme, ina almasi 1,354 na zumaridi 56, kulingana na maelezo yaliyotumwa mtandaoni na Louvre. Hali yake “iko chini ya uchunguzi,” Wizara ya Utamaduni imesema.

Moja ya  skuta zilizotumiwa na wahalifu hao pia ilipatikana.

Tunajua nini kuhusu wahalifu? Mapema jioni, kwenye BFMTV, mwendesha mashtaka wa Paris alitangaza kuwa “komando” wa watu wanne walikuwa wanatafutwa. Wanaume hawa wanne walijificha nyuso zao wakati wa wizi na wakakimbia “kwa skuta zenye nguvu kubwa,” amesema Laure Beccuau, ambaye pia ametaja uwezekano wa kuwepo kwa “wafadhili” na “wahusika wa dogo” ndani ya kundi hili la uhalifu.

Hapo awali, Laurent Nuñez alisema kuwa wizi huo ulifanywa na “timu yenye uzoefu mkubwa” na akabainisha kwamba wezi hao wanaweza kuwa “wageni.” Uchunguzi kuhusu wizi uliopangwa na njama za kutenda uhalifu umefunguliwa na kukabidhiwa kwa Brigedi ya Kuzuia Ujambazi (BRB), ofisi ya mwendesha mashtaka wa Paris imetangaza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *