#IRAN
Katika saa moja iliyopita, vyombo kadhaa vya habari vimeripoti kuwa mjumbe maalum wa Donald Trump, Steve Witkoff, pamoja na Jared Kushner, wamekuwa wakifanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Iran, Mohammad-Bagher Ghalibaf, wakinukuu vyanzo mbalimbali.

Hata hivyo, sasa akaunti ya X inayohusishwa na Mohammad-Bagher Ghalibaf imetangaza kuwa hakujakuwa na mazungumzo yoyote na Marekani.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa “habari za uongo” zimetumika “kuathiri na kupotosha masoko ya mafuta”, na kwamba wananchi wa Iran “wanataka wahusika wa mashambulizi waadhibiwe kikamilifu na kwa majuto.”

#CHANZOBBCSWAHILI
#starTvUpdate

(Feed generated with FetchRSS)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *