Chanzo cha picha, EPA
Rais wa
Ukraine Volodymyr Zelensky aliwasili Saudi Arabia siku ya Alhamisi, baada ya
kusema mapema kwamba ndege zisizo na rubani za Ukraine zinaweza kusaidia
kuboresha usalama katika eneo la Ghuba.
“Mikutano
muhimu imepangwa. Tunashukuru usaidizi wa wale walio tayari kufanya kazi nasi
ili kuhakikisha usalama, na tunawaunga mkono pia”, alisema katika ujumbe
kwenye mitandao ya kijamii.
Mapema siku
ya Alhamisi, Zelensky alitoa utaalamu wa Ukraine katika teknolojia ya ndege
zisizo na rubani kama njia ya kuboresha usalama kote ulimwenguni, haswa eneo la
Ghuba.
“Hili
ni muhimu kwa sababu usalama wa nishati – na gharama ya maisha, haswa barani
Ulaya – inategemea mafuta, gesi na rasilimali zingine, na masoko thabiti ya
kimataifa,” alisema katika ujumbe wa video kwa Kikosi cha Pamoja cha
Usafirishaji, muungano wa usalama ambao ulifanya mkutano wa kilele huko
Helsinki.
“Cha
msingi si tu kutengeneza silaha mpya – hasa ndege zisizo na rubani – si
teknolojia tu, bali pia uzoefu halisi katika kuzitumia, na kuziunganisha na
rada, usafiri wa anga, na mifumo mingine ya ulinzi wa anga. Tuna uzoefu
huu,” alisema.
Zelensky
alisema kwamba kwa mabadilishano anatafuta msaada wa kuilinda Ukraine dhidi ya
uvamizi unaoendelea wa Urusi.
“Tungependa
mataifa ya Mashariki ya Kati pia yatupe fursa ya kujiimarisha. Yana makombora
fulani ya ulinzi wa anga ambayo hatuna ya kutosha. Hilo ndilo tungependa
kufikia makubaliano,” alisema katika mahojiano na gazeti la Ufaransa la Le
Monde.
Soma zaidi: