Wakati kundi hilo lenye silaha likizidisha mashambulizi yake katika jimbo hili la kaskazini mashariki mwa DRC kwa wiki kadhaa, angalau vijiji vinne magharibi mwa jiji la Bunia vilishambuliwa tena Jumamosi, Machi 28, na Jumapili, Machi 29. Ingawa idadi ya vifo kutokana na shambulio hili bado haijulikani, raia kadhaa, ikiwa sio mamia kadhaa, walitekwa nyara na washambuliaji.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mashambulizi haya mapya yanayohusishwa na kundi lenye silaha la Allied Democratic Forces (ADF) yaliripotiwa mwishoi mwa wiki hii iliyopita huko Ituri, mkoa ulio kaskazini mashariki mwa DRC. Katika muda wa saa 48, angalau vijiji vinne magharibi mwa Bunia, kwenye barabara ya Mambasa-Komanda, vililengwa.

Shambulio hilo lilianza Jumamosi, Machi 28, katika kijiji cha Babungwe, kilichopo katika eneo la Mambasa, na kusababisha hofu na watu kuhama makazi yao.

Ingawa hakuna takwimu za majeruhi zinazopatikana katika hatua hii, raia wengi wamechukuliwa mateka na ADF, kulingana na John Vuleverio, mwanaharakati wa haki za binadamu. “Kumekuwa na visa vingi vya utekaji nyara. Baada ya kupora maduka na biashara kwa kiasi kikubwa, washambuliaji waliwachukua raia kusafirisha nyara vitu hivyo walivyopora ndani kabisa ya msitu,” alisema.

Takriban mateka mia moja tayari wameachiliwa huru, kulingana na jeshi la Kongo.

Pia kulingana na mashirika ya kiraia, ADF pia imeongeza mashambulizi yake katikamkoa huo katika wiki za hivi karibuni. Katika eneo la Mambasa pekee, zaidi ya mashambulizi kumi yamerekodiwa katika kipindi cha mwezi mmoja. Mwanzoni mwa mwezi Machi, maeneo mawili ya migodi yalilengwa, na kusababisha vifo vya angalau watu kumi na saba.

Jioni ya Jumatatu, Machi 30, msemaji wa jeshi huko Ituri, Luteni Jules Ngongo, alisema kwamba shughuli zinaendelea katika eneo hilo na kwamba takriban mateka mia moja tayari wameachiliwa huru.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *