WABUNGE kutoka Baraza la Wawakilishi (BLW) wameapishwa leo jijini Dodoma na kuahidi kusimamia maslahi ya wananchi wa pande zote za Muungano kwa kuzingatia vipaumbele vya maendeleo.

Wakizungumza baada ya kuapishwa, baadhi ya wabunge hao wamesema watahakikisha wanakuwa sauti ya wananchi ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kujali wanatoka Tanzania Bara au Visiwani. Miongoni mwao ni Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu, Simai Mohamed Said, ambaye amesema atahakikisha anasimamia masuala ya maendeleo yanayogusa wananchi moja kwa moja.

Hatahivyo , amesema atazingatia sekta muhimu zikiwemo utalii, fedha na miundombinu ili kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wananchi. Naye Mwakilishi wa Jimbo la Gando, Said Ali Mbarouk, amesema ataweka mkazo katika kuwasemea wananchi wake na kuhakikisha changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi kupitia vyombo vya maamuzi.

Amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya pande mbili za Muungano ni muhimu katika kuleta maendeleo endelevu na yenye manufaa kwa wananchi wote. Wabunge hao wmeeleza kuwa watafanya kazi kwa karibu na Serikali kuhakikisha sera na mipango inayopitishwa inaleta tija na ustawi wa wananchi nchini. SOMA: Serikali yaongeza kasi elimu, afya na ajira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *