
Marekani inafikiria “mazungumzo ya ana kwa ana” na Iran, msemaji wa Ikulu ya White House Karoline Leavitt amesema, baada ya Washington na Tehran kukubaliana kusitisha mapigano kwa wiki mbili badala ya kufunguliwa tena kwa Mlango-Bahari wa Hormuz.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Majadiliano yanaendelea kuhusu mazungumzo ya ana kwa ana, lakini hakuna uamuzi utakaochukuliwa hadi rais au Ikulu ya White House itakapotangaza,” ameongeza.
Mazungumzo kati ya pande hizo mbili yamepangwa kuanza Ijumaa, Aprili 10, huko Islamabad, Pakistan.
Wakati huo huo Ikulu ya White House imesema Israel imekubali kusitisha mapigano na Iran.
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina, afisa wa Ikulu ya White House ameliambia shirika la habari la AFP kwamba Israel imekubali kusitisha mapigano baada ya Marekani na Iran kukubaliana kusitisha mapigano.