Ofisi ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu imesema Jumatano kwamba makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyoratibiwa na Marekani na Iran “hayaijumuishi Lebanon,” ambayo iliingizwa katika vita vya Mashariki ya Kati kufuatia mashambulizi ya kundi linalounga mkono Iran la Hezbollah dhidi ya Israel.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Usitishaji mapigano wa wiki mbili hauijumuishi Lebanon,” ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel imesema katika taarifa kwa waandishi wa habari.

Taarifa hii inapingana na tangazo la awali la Waziri Mkuu wa Pakistani Shehbaz Sharif, mpatanishi katika mzozo huo, ambaye alisema kwamba usitishaji mapigano unatumika “kila mahali, ikiwa ni pamoja na Lebanon na kwingineko.”

Wakati vita katika Mashariki ya Kati vikiendelea kwa siku yake ya 40, Washington na Tehran, siku ya Jumanne, Aprili 7, zilikubaliana kusitisha mapigano kwa wiki mbili badala ya kufunguliwa tena kwa Mlango-Bahari wa Hormuz. 

Wakati huo huo jeshi la Israeli, kwa upande wake, lilifanya “mfululizo mpana wa mashambulizi siku ya Jumanne likilenga maeneo kadhaa ya miundombinu ya utawala wa kigaidi wa Iran katika maeneo kadhaa kote Iran,” kulingana na taarifa ya kijeshi ya Israel. Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Volker Türk alibainisha kwamba “kushambulia raia na miundombinu ya raia kimakusudi ni uhalifu wa kivita.”

Jeshi la Israeli pia lilitangaza kwamba limekamilisha kupelekwa kwa wanajeshi wake wa ardhini kusini mwa Lebanon kwenye “safu ya ulinzi ya hali ya juu” dhidi ya wapiganaji kutoka kundi la Hezbollah.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *