Waziri Mkuu wa Uhispania Pedro Sánchez, akizungumza mjini Beijing siku ya Jumatatu, Aprili 13, 2026, amekosoa faida ya biashara “isiyo endelevu” ya China na Umoja wa Ulaya, ambayo aliielezea kama chanzo cha “mateso ya kijamii” na tabia za “kujitenga”.

Imechapishwa:

Dakika 3 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Katika hotuba yake mjini Beijing, Waziri Mkuu wa Uhispania, alitoa wito kwa China kufunguka zaidi kwa biashara ya Ulaya

“Umoja wa Ulaya unafanya sehemu yake […] Tunahitaji China kufanya vivyo hivyo. Inahitaji kufunguka ili Ulaya isilazimike kujitenga,” amesema.

Pedro Sanchez ametoa wito kwa China kufunguka zaidi kwa biashara ya Ulaya katika hotuba aliyoitoa katika Chuo Kikuu cha Tsinghua.

“Umoja wa Ulaya unafanya sehemu yake… Tunahitaji China kufanya vivyo hivyo. Inahitaji kufunguka ili Ulaya isilazimike kujitosheleza yenyewe,” alisema.

EU inahitaji China “kutusaidia kurekebisha nakisi ya biashara tuliyo nayo, nakisi isiyo na usawa ambayo iliongezeka kwa 18% nyingine mwaka jana na haiwezi kudumu kwa jamii zetu kwa muda wa kati na mrefu,” alisema.

Nakisi ya biashara na China inawakilisha 74% ya nakisi yote ya Uhispania, ameelezea.

“Hali hii haiwezi kudumu kwa sababu ya harakati za kujitenga inazokabiliana nazo na chuki na mateso ya kijamii ambayo husababisha,” aliongeza.

Bw. Sanchez alianza programu rasmi ya ziara yake ya siku tatu nchini China katika Chuo Kikuu cha Tsinghua, ziara yake ya nne nchini humo baada ya miaka minne.

Kiongozi huyo wa kisoshalisti, ambaye yuko madarakani tangu mwaka 2018, ndiye kiongozi wa hivi karibuni wa Magharibi kufanya ziara hiyo katika miezi ya hivi karibuni, kwa nia ya kuimarisha uhusiano na China licha ya kutokuwa na uhakika unaotokana na vitendo vya Marekani.

Rais wa Marekani Donald Trump alitishia mwezi uliopita kukomesha biashara na Uhispania wakati Madrid ilipokataa kuruhusu matumizi ya kambi zake za kijeshi kwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya Iran. Bw. Trump anatarajiwa nchini China katikati ya mwezi Mei.

Pedro Sanchez anatafuta kuiweka Uhispania kama mpatanishi kati ya Beijing na Umoja wa Ulaya. Anatarajiwa kukutana na Rais wa China Xi Jinping siku ya Jumanne.

Wazungu wana wasiwasi na ukubwa wa nakisi ya biashara dhidi yao. Wana wasiwasi kuhusu China kuijaza Ulaya na uzalishaji wake wa ziada kwa gharama nafuu. Pia wameshutumu kwa muda mrefu vikwazo vilivyowekwa katika njia ya kufikia soko la China.

Siku ya Jumatatu, Bw. Sanchez ametoa ombi kwa ajili ya Ulaya. Ameitaka China isidharau uzito wa EU, kambi inayoongoza ya biashara duniani, nchi ya pili kwa uchumi mkubwa duniani, na mpokeaji mkubwa zaidi wa uwekezaji wa moja kwa moja wa nchi za kigeni duniani, amebainisha.

Pia alitumia lugha aliyoijua Wachina wakisikiliza kwa makini, akielezea Ulaya kama mdau katika “utulivu” wa kimataifa katika ulimwengu wenye matatizo na kutetea kuimarishwa kwa ushirikiano wa pande nyingi na mageuzi ya Umoja wa Mataifa.

Kwa Madrid, moja ya malengo makuu ya ziara hiyo ni kupata ufikiaji bora wa soko la China, haswa kwa bidhaa za kilimo na viwanda, na kuchunguza mikataba ya pamoja katika sekta ya teknolojia, vyanzo vya serikali ya Uhispania vimeliambia shirika la habari la AFP.

– Uhispania “rafiki” –

Pedro Sanchez pia anatarajiwa kutumia ziara yake kuvutia wawekezaji wapya katika nch hii ya nne yenye uchumi mkubwa katika ukanda wa euro na kupata ufikiaji bora wa malighafi za China zinazotafutwa sana.

Uhispania ilirekodi nakisi ya biashara ya euro Bilioni 42.3 na China mnamo 2025.

Serikali inasema kwamba mauzo ya nje ya Uhispania kwenda China yaliongezeka kwa 6.8% mnamo mwaka 2025, ikihusisha ukuaji huu na nguvu ya uhusiano na Beijing.

Wakati wa ziara ya Pedro Sanchez nchini China mnamo mwezi Aprili 2025, Beijing ilikubali kupanua ufikiaji wa soko kwa bidhaa mbalimbali za Uhispania, ikiwa ni pamoja na nyama ya nguruwe na matunda ya cheri .

Uhispania inawavutia wawekezaji wa China, hasa kwa sababu uchumi wake unajivunia mojawapo ya viwango vya juu zaidi vya ukuaji barani Ulaya na gharama za nishati zinaendelea kuwa chini kwa kiasi, anaelezea Claudio Feijoo, mtaalamu wa China katika Chuo Kikuu cha Ufundi cha Madrid (UPM).

“China inaiona Uhispania kama rafiki kwa kiasi, isiyo na migogoro mingi kuliko nchi zingine, na labda huru zaidi kwa Washington. Hii inawezesha kufanya maamuzi kwa uhuru zaidi,” ikimaanisha kuwa nje kidogo ya mipaka ya makubaliano ya Ulaya, ameliambia shirika la habari la AFP.

“Uhispania pia inaonekana kama lango la Ulaya, Amerika Kusini, na Afrika Kaskazini,” mtaalamu huyo amesema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *