Rais wa Marekani Donald Trump amezungumza na mwenzake wa Lebanon, Joseph Aoun, na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu siku ya Alhamisi, Aprili 16.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Rais Donald Trump ametangaza kwenye mtandao wake wa Truth Social kwamba Lebanon na Israel zimekubaliana kusitisha mapigano kwa siku kumi.

Katika mtandao wake wa Truth Social, Donald Trump ametangaza kwamba amezungumza na Joseph Aoun, rais wa Lebanon, na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu. Kulingana na rais wa Marekani, Israeli na Lebanon zimekubaliana kusitisha mapigano kwa siku 10.

Majadiliano kati ya viongozi wa Marekani, Lebanon, na Israel yamefanyika mchana, hasa kwa lengo la kufikia makubaliano ya kusitisha mapigano. Hata hivyo, Rais wa Lebanon Joseph Aoun alikataa kukutana na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.

Donald Trump ametangaza kuwa atawaalika Benjamin Netanyahu na Joseph Aoun Ikulu ya White House.

Wakati huo huo ikulu ya Élysée imesema inakaribisha “habari nzuri” ambazo zitahitaji “kuthibitishwa katika maeneo yaliyokuwa yamekumbwa na mapigano.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *