Jeshi la Israel limeagizwa kumuua mpiganaji yeyote wa Hezbollah katika eneo la kusini mwa Lebanon linaloanzia mpaka wa Israel na Lebanon hadi Mto Litani, ambao unapita takriban kilomita 30 (maili 19) kaskazini, kulingana na taarifa ya kijeshi iliyotolewa siku ya Jumatano Aprili 15, 2026.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

“Nimetoa amri ya kugeuza eneo la kusini mwa Lebanon hadi Mto Litani kuwa eneo kuangamiza gaidi yeyote wa Hezbollah,” kundi la Kishia la Lebanon linaloshirikiana na Tehran, taarifa imebainisha, ikimnukuu Luteni Jenerali Eyal Zamir, mkuu wa jeshi, wakati akizuru wanajeshi wa Israel waliotumwa nchini Lebanon.

Kundi la Hezbollah limesema uamuzi wa serikali ya Lebanon kufanya mazungumzo na Israel ulikuwa dhambi ya kitaifa ambayo ingeongeza mgawanyiko nchini Lebanon

Wakati huo huo kundi la Hezbollah limesema uamuzi wa serikali ya Lebanon kufanya mazungumzo na Israel ulikuwa dhambi ya kitaifa ambayo ingeongeza mgawanyiko nchini Lebanon, likisisitiza mpasuko mkubwa uliopo huku kundi hilo linaloungwa mkono na Iran likiendelea kupigana vita na Israeli.

Mbunge wa Hezbollah, Hassan Fadlallah, amesema mkutano wa Jumanne uliosimamiwa na Marekani kati ya balozi wa Lebanon mjini Washington na mwenzake wa Israel haukuonyesha utambulisho wa kitaifa wa Lebanon au ari na chaguo la watu wake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *