Kufuatia vurugu za kikabila zilizosababisha vifo vya watu kadhaa kuanzia Jumamosi hadi Jumatatu—angalau watu 42 kulingana na hesabu rasmi, karibu 60 kulingana na vyanzo vya kuaminika—Rais wa Chad Mahamat Idriss Déby yuko katika eneo la Dar Tama la katika mkoa wa Wadi Fira mashariki mwa Chad tangu Jumanne jioni. Anasisitiza kwamba lengo la serikali ni kulinda mpaka na Sudan na kuwanyang’anya silaha raia.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Akiwa amevaa sare ya jeshi, Mahamat Idriss Déby alitaka kuonyesha mamlaka yake tangu aliposhuka kutoka kwenye helikopta huko Igot. Alikutana na viongozi mbalimbali katika eneo hilo, viongozi wa kimila, na viongozi wa kijeshi, pamoja na ujumbe wa serikali uliokuwepo tangu Jumapili, Aprili 26, kujaribu kutuliza hali iliyotokana na mzozo kuhusu kisima kati ya wanawake kutoka jamii za Tama na Zaghawa. Mgogoro huo uliongezeka baada ya kuwasili kwa wanamgambo wa Sudan wa Zaghawa waliovuka mpaka wakiwa na silaha na magari yao.

Kulingana na vyanzo vya kuaminika, mkuu wa nchi anatafuta kutumia njia ya imila ili kutatua mgogoro huko Igot. Kulingana na taarifa rasmi kutoka kwa ofisi ya rais wa Chad, maeneo yote mashariki yanakabiliwa na hatari ya vita kuenea hadi Sudan, kwa hivyo vipaumbele ni kulinda mpaka na kuwanyang’anya silaha raia.

Mahamat Idriss Deby amekuwa na tabia ya kutembelea maeneo yaliyoathiriwa na migogoro ya ndani, lakini waangalizi wengi wanaona uwepo wake kama “kuwafumba macho raia” na wana wasiwasi kuhusu ukosefu wa suluhisho la serikali kwa matatizo ya msingi yanayosababisha aina hii ya vurugu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *