DRC: Sintofahamu yazuka katika kituo cha matibabu cha Rwampara, mahema mawili yateketezwa motoDRC: Sintofahamu yazuka katika kituo cha matibabu cha Rwampara, mahema mawili yateketezwa moto

Huko Rwampara, yapata kilomita kumi kutoka Bunia, ndugu wa mgonjwa aliyefariki kutokana na Ebola wameteketeza mahema katika kituo cha matibabu siku ya Alhamisi, Mei 21, 2026, baada ya wafanyakazi wa matibabu kukataa kuwakabidhi mwili wa marehemu. Waziri wa Afya Roger Kamba amesthumu kilichotokea.  

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Asubuhi: afisa wa Alima anaelezea vituo vilivyoshambuliwa na watu wnye hasira

Barry Mamadou Kaba, mkuu wa misheni wa shirika lisilo la kiserikali la Alima nchini DRC, alikuwa tayari ameelezea hali ngumu kwenye RFI. Huko Rwampara, wagonjwa waligawanywa kati ya vituo viwili: hospitali kuu na CME, kituo cha kibinafsi cha jirani. Alima ilikuwa imeweka mahema haraka ili kutenganisha wagonjwa wanaoshukiwa kuambukizwa virusi vya Ebola na wagonjwa wengine na kuwalinda wafanyakazi wa afya.

“Mahitaji ni makubwa,” alisema Barry Mamadou Kaba. Ili kujenga kituo sahihi cha matibabu ya Ebola, chenye mizunguko iliyorekebishwa, nafasi za kibinafsi, na ulinzi wa kutosha kwa wauguzi na wagonjwa, inahitaji uwezo wa kifedha. Uwezo ambao washirika hawana kwa sasa. Ikiwa fedha zitafika, Barry Mamadou Kaba anakadiria, kituo hicho kinaweza kuwa tayari baada ya wiki moja.

Alima pia ilikuwa imesafirisha “vibanda” vyake hadi Bunia: vyumba vya dharura vilivyo salama kibiolojia ambavyo vinaruhusu kila mgonjwa kutengwa mmoja mmoja huku wakidumisha utu wao kwa kumlinda muuguzi. Huko Rwampara, wakati huo Barry Mamadou Kaba alikuwa akizungumza, wagonjwa watano wanaoshukiwa kuambukizwa virusi vya Ebola na mgonjwa mmoja aliyethibitishwa kuambukizwa virusi hivyo walikuwa wakifuatiliwa katika hospitali kuu.

Alasiri kulitokea tukio baya 

Kabla ya siku hiyo kuisha, mgonjwa ambaye alikuwa amepimwa na kupatikana na virusi vya Ebola alifariki katika kituo cha matibabu cha Rwampara. Marafiki zake, waendesha pikipiki, walijaribu kuuchukua mwili wake. Timu za matibabu zilielezea hatari na kujaribu kuwazuia, lakini bila mafanikio. Wanaume hao walichoma moto mahema mawili.

Anachoelezea Waziri Afya wa DRC

Roger Kamba, Waziri wa Afya, alijibu mara moja alipohojiwa na RFI. Ebola haiambukizwi kama UVIKO-19: si ugonjwa wa kupumua. Virusi huambukizwa kupitia kugusana na majimaji ya mwili: damu, mkojo, kinyesi, matapishi, na jasho. Majimaji haya yote yana virusi. Mwili wa mtu ambae amefariki kutokana na virusi vya Ebola unaendelea kuambukiza. Mtu yeyote anayeugusa bila kinga ana hatari ya kuambukizwa. ” Tafadhalini mtupe nafasi ya kumzika marehemu salama,” alisema Roger Kamba. “Mtu aliyefariki hawezi kusababisha wengine kupoteza maisha.” 

Jibu la Alima

Alima inalaani kuhatarisha maisha ya binadamu na uharibifu wa vifaa muhimu vya matibabu. Shirika hilo lisilo la kiserikali linaonya kuhusu kuenea kwa taarifa ambazo hazijathibitishwa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii, ambazo zinaweza kuchochea hofu na kutoaminiana kwa wafanyakazi wa afya. Katika muktadha nyeti kama huo, inasema, usambazaji wa taarifa zilizothibitishwa ni muhimu ili kulinda raia na kuhakikisha upatikanaji wa huduma.

Hatua za haraka zimetekelezwa: upangaji upya wa muda wa nafasi za huduma ya afya, kuhakikisha shughuli za kimatibabu, ugawaji upya wa vifaa muhimu, na maandalizi ya suluhisho mbadala ili kuhakikisha mwendelezo wa huduma.

Mahitaji ya eneo husika

Tukio la Rwampara linatokea katika muktadha wa upungufu wa uwezo ambao umeshuhudiwa kwa siku kadhaa. Huko Bunia, Florent Uzzeni, naibu mkuu wa dharura wa Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) kutoka Uswisi, ambaye aliwasili siku mbili mapema, alieleea hali hiyo. Vituo vinavyohudumia wagonjwa vimejaa. Hospitali, vituo vya afya, kliniki za kibinafsi: hakuna kitanda hata kimoja kinachopatikana. “Hakuna hatua madhubuti zilizochukuliwa. Bado kuna kazi nyingi ya kufanya,” aliiambia RFI.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *