Kingozi wa Kanisa Katoliki duniai, Papa Leo XIII, amekutana na waathiriwa sita wa unyanyasaji wa kingono uliofanywa na makasisi Wakatoliki nchini Uhispania, Vatican imetangaza. Makundi ya waathiriwa ambao hawakualikwa yalikosoa mkutano huo, yakiuita kama operesheni rahisi ya mawasiliano.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Vatican imetoa maelezo machache kuhusu mkutano huo, ambao ulidumu kwa takriban saa moja. Hata hivyo, imebainisha kwamba Leo XIII alisikiliza mapendekezo yaliyolenga kuimarisha ulinzi wa waathiriwa ndani ya Kanisa na kuahidi kuifanya iwe mahali salama kwa kila mtu.

Wakati wa ziara rasmi ya wiki moja nchini Uhispania, Leo XIII hapo awali alishughulikia kwa mara ya kwanza kashfa ambazo zimetikisa uaminifu wa Kanisa la Uhispania, akiwaambia maaskofu kwamba lazima wawasikilize waathiriwa na kuwalipa fidia.

Papa alisikiliza mapendekezo ya kuboresha ulinzi wa waathiriwa na kuwahakikishia makasisi kwamba waathiriwa wanapaswa kuona ahadi kutoka kwa Kanisa kuhusu usalama wao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *