
Nchini Burkina Faso, utawala wa kijeshi umetangaza Ijumaa jioni, Juni 26, 2026, kwamba unavunja mahusiano yake ya kidiplomasia na Ufaransa. Tangazo hilo lilitolewa kwenye televisheni ya taifa na msemaji wa serikali PingdwendĂ© Gilbert OuĂ©draogo. Burkina Faso ililaani, haswa, “harakati zisizoisha” za Ufaransa dhidi ya maslahi yake, kufuatia miaka kadhaa ya mvutano kati ya nchi hizo mbili. Ufaransa ilijibu, ikisema “inasikitishwa” na uamuzi wa “uhasama na usio na msingi.”
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Siku ya Ijumaa, Juni 26, 2026, utawala wa kijeshi nchini Burkina Faso ulitangaza kuwa unavuja mahusiano yake ya kidiplomasia na Ufaransa. Serikali ilisema kwamba “masharti muhimu ya kukuza mahusiano yanayotegemea heshima ya pande zote, uaminifu wa pande zote, na kanuni ya kutoingilia kati” hayatimizwi tena katika mahusiano yake ya kitaasisi na Paris.
Ouagadougou inaishutumu Ufaransa kwa “kampeni zisizookoma dhidi ya maslahi ya Burkina Faso, na matarajio ya ukoloni mamboleo na “kibeberu”. Serikali ya Burkina Faso pia inaishutumu Paris kwa kuunga mkono “mitandao ya uasi” na “magaidi […] wanaosababisha vifoi kwa Sahel.” Pia inalalamika kuhusu kampeni ya kuihujumu nchi na kuifanya nchi hiyo “isipendwi na jumuiya ya kimataifa”.
Katika taarifa, serikali ya Burkina Faso inabainisha kwamba kuvunjika kwa na Ufaransa “kunahusu uhusiano wao wa kidiplomasia pekee” lakini “haivunji uhusiano wa kihistoria kati ya watu hao wawili.”
Ufaransa inasikitishwa na uamuzi “wa uadui” na “usio na msingi” Baadaye jioni ya Ijumaa, Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa ilijibu. Paris “inasikitishwa” na “uamuzi wa uadui na usio na msingi” wa utawala wa kijeshi wa Burkina Faso. “Uamuzi huu wa pande zote mbili” “unaonyesha hali ya wasiwasi ya mamlaka ya Burkina Faso” Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa iliongeza, ikibainisha kuwa “hatua muhimu za pande zote zinapitiwa upya kwa sasa.”
Burkina Faso iliomba kuondoka kwa balozi wa Ufaransa mapema mwaka wa 2023 na baadaye ikakataa kuidhinisha mwanadiplomasia mpya. Tangazo la Ijumaa sasa linafungua njia ya kusitishwa haraka kwa shughuli zote za kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.
Ufaransa inasema inatilia maanani sana “usalama wa wafanyakazi wa serikali” na “raia wa Ufaransa” waliopo Burkina Faso.