Safari za ndege kati ya Comoro na Madagascar zinatarajiwa kuanza tena mwezi huu wa Julai, baada ya kusitishwa kwa takriban miaka minne. Tangazo hilo lilithibitishwa jana Jumatatu, Julai 6, na Rais Azali Assoumani wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wa Comoro. Kuanza tena kwa safari hizi kunasubiriwa kwa hamu na wasafiri, wanafunzi, na wafanyabiashara katika nchi zote mbili.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Moroni, Abdallah Mzembaba

Tangazo la kuanza tena kwa safari za ndege linakuja baada ya miaka kadhaa ya mvutano wa kidiplomasia kati ya Moroni na Antananarivo, haswa dhidi ya msingi wa mzozo kuhusu kilo 49 za dhahabu zilizokamatwa Comoro mnamo mwezi Desemba 2021 na kurejeshwa mwezi Machi 2025, kufuatia “makubaliano ya pande zote mbili” kati ya nchi hizo mbili. Mnamo mwezi Julai 2022, Madagascai ilisitisha safari za ndege na Comoro, ikitaja rasmi sababu za kiafya.

Kulingana na Soilihi Mohamed Djounaid, Naibu Katibu Mkuu wa Serikali, mahusiano yaliyoanzishwa wakati wa ziara ya hivi karibuni ya Azali Assoumani nchini Madagascar kwa ajili ya sikukuu ya kitaifa yalisaidia kutatua suala hili: “Tunaweza kusema kwamba kumeanzishwa uhusiano wa ushirikiano, urafiki, na udugu na mamlaka mpya ya Madagascar.” Miongoni mwa mambo yaliyokubaliwa na pande zote mbili ni kuanza tena mara moja kwa safari za ndege. Mamlaka ya Madagascar inabainisha kuwa safari hizi zitaanza mwezi Julai. Sijawa tarehe maalum bado. “

Nourdine Saïd aliishi Madagascar kwa miaka minne na anakaribisha habari hii: “Ni habari njema kwa sababu tulilazimika kupitia Addis Ababa ili kufika maeneo karibu na nyumbani. Bila shaka, hii itapunguza nauli za ndege kwa sababu safari za mkato zinagharimu pesa nyingi ikilinganishwa na safari ya ndege ya moja kwa moja. Tutafanya biashara. Kila mtu atanufaika.”

Kuanza tena kwa safari sasa kunakubaliwa kisiasa, lakini utaratibu wake bado unahitaji maelezo zaidi, ikiwa ni pamoja na tarehe halisi na shirika la ndege.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *