• Mshambuliaji wa pembeni wa Ureno, Pedro Neto, alionekana akicheza dhidi ya Hispania akiwa amevaa viatu vilivyokuwa na tundu kubwa karibu na kisigino, jambo lililowashangaza mashabiki waliokuwa wakitazama mechi ya hatua ya 16 Bora ya Kombe la Dunia
  • Mashabiki wengi wamezoea kuona wachezaji wakikata soksi zao, lakini kukata kiatu chenyewe ni jambo nadra sana na lilizua mshangao mkubwa mtandaoni
  • Tunaeleza sababu ya mabadiliko hayo yasiyo ya kawaida kwenye viatu, ambayo ni njia ya matibabu ya tatizo la mfupa unaoota nyuma ya kisigino na kusababisha maumivu

Mashabiki waliokuwa wakitazama Ureno ikicheza dhidi ya Hispania katika mechi ya hatua ya 16 Bora ya Kombe la Dunia la FIFA 2026 mnamo Julai 6 walipata jambo la kushangaza ambalo halikuhusiana na matokeo ya mwisho ya mchezo.

Pedro Neto alicheza na tundu kwenye buti zake, Kwa Nini Wacheza Kandanda Walikata Matundu Katika Buti Zao za KSh 44,000?
Pedro Neto alicheza na shimo kwenye buti zake. Picha na Catherine Ivill.
Source: Getty Images

Pedro Neto alionekana uwanjani akiwa amevaa viatu vilivyokuwa na tundu kubwa lililokatwa karibu na kifundo cha mguu, huku soksi yake ikionekana wazi kupitia tundu hilo.

Picha hiyo ilisambaa kwa kasi na kuwafanya watazamaji wengi kujiuliza sababu ya mabadiliko hayo.

Pia soma

“Tuliponea chupuchupu”: Familia ya Kakamega yasimulia dakika za kutisha baada ya ajali ya Tahmeed

Ureno baadaye ilipoteza mechi hiyo kwa mabao 1-0, lakini viatu hivyo vya ajabu tayari vilikuwa vimezua mjadala mkubwa mtandaoni.

Kwa nini wachezaji hukata viatu vyao?

Mashabiki wengi wa soka wamewahi kuona wachezaji wakikata soksi zao wakati wa mechi ili kupunguza shinikizo au kuboresha mzunguko wa damu kwenye sehemu ya chini ya mguu.

Hilo ni jambo linalojulikana sana katika mchezo wa soka.

Hata hivyo, kukata kiatu chenyewe ni jambo nadra zaidi, na ndiyo sababu hali ya Neto ilivutia macho ya wengi.

Kwa mujibu wa The Athletic, mabadiliko hayo si ya urembo bali ni ya kitabibu.

Sababu yake ni hali inayojulikana kama Haglund’s deformity, ambayo pia huitwa kwa jina la utani “pump bump.”

Sababu ya wachezaji wa soka kukata matundu kwenye viatu vyao yafafanuliwa
Pedro Neto alikata buti zake kwenye Kombe la Dunia la 2026. Picha na Hannah Peters.
Source: Getty Images

Hali hiyo husababisha mfupa kujitokeza nyuma ya kisigino.

Sehemu ngumu ya nyuma ya kiatu cha soka inapobana sehemu hiyo mara kwa mara, inaweza kusababisha maumivu makali na uvimbe kwenye Achilles tendon pamoja na bursa, mfuko mdogo wenye majimaji unaolinda eneo hilo.

Kwa kukata sehemu hiyo ya kiatu, wachezaji huondoa kabisa shinikizo linalosababisha maumivu hayo, jambo linalowawezesha kuendelea kucheza katika kiwango cha juu bila kuzidisha jeraha.

Pia soma

Mwanamke wa Nairobi anayetuhumiwa kumchoma kisu hadi kumuua mpenziwe Pipeline asimulia kilichotokea

Ni wachezaji gani wengine wamekata mashimo kwenye viatu vyao?

Pedro Neto si mchezaji wa kwanza maarufu kutumia mbinu hiyo.

Roberto Firmino na Philippe Coutinho pia waliwahi kuonekana wakivaa viatu vilivyokatwa kwa mtindo kama huo wakati wa mechi.

Kwa mwonekano, viatu hivyo huonekana vya kipekee, vikifanana na mchanganyiko wa kiatu cha kawaida na kandambili.

Hata hivyo, kwa wachezaji wanaokabiliwa na maumivu ya kisigino, suluhisho hilo linaonekana kuwa na manufaa makubwa kuliko mwonekano wake.

Kwa nini wachezaji wa Hispania hawaimbi wimbo wa taifa?

Pia tuliangazia sababu zinazowafanya wachezaji wa Hispania kubaki kimya wakati wimbo wao wa taifa, La Marcha Real, unapopigwa kabla ya mechi za kimataifa.

Kutokuwepo kwa maneno katika wimbo huo, hali iliyotokana na mabadiliko ya kihistoria na misukosuko ya kisiasa, huongeza maana ya heshima yao ya kimya kabla ya kushuka dimbani.

Makala haya yamedhaminiwa kwa fahari na 1XBet.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.

Chanzo: TUKO.co.ke

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *