Baada ya kukutana na Rais wa Kongo Félix Tshisekedi huko Kinshasa siku ya Alhamisi, Januari 29, viongozi watano wa zamani wa Afrika wanaounda jopo la waratibu wa Umoja wa Afrika kwa mashariki mwa DRC wanatarajiwa kukutana na Rais wa Rwanda Paul Kagame leo Ijumaa. Kisha watasafiri kwenda Burundi kabla ya kuwasilisha ripoti kuhusu dhamira yao katika mkutano ujao wa Umoja wa Afrika huko Addis Ababa katikati ya mwezi Februari.

Imechapishwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Hali mashariki mwa DRC ilikuwa lengo la mkutano kati ya waratibu wa Umoja wa Afrika (AU) na Rais wa Kongo Félix Tshisekedi, ambaye aliwapokea Kinshasa, akiandamana na timu ya upatanishi ya Togo, siku ya Alhamisi, Januari 29. Lengo la jopo hili, linaloundwa na wakuu watano wa zamani wa nchi za Afrika, waliopewa jukumu na AU la kuunga mkono michakato ya amani ya Washington na Doha? “Ili kufikia utulivu, kudumisha mazungumzo, na kufanya kazi kuelekea maridhiano kati ya pande hizo,” kinaelezea chanzo kilicho karibu na faili hiyo. Kazi yake ni “kupata suluhu za Kiafrika kwa matatizo ya Afrika,” mwanadiplomasia aliyeko DRC amemwambia mwandishi wetu wa habari aliyeko mjini Kinshasa, Paulina Zidi.

Ujumbe huo unatarajiwa kuwasilisha ripoti kwa AU yenye mapendekezo kadhaa, ambayo yatawasilishwa katika mkutano ujao wa shirika hilo katikati ya mwezi Februari huko Addis Ababa. “Tutasikiliza kila mtu na kuona kinachoweza kufanywa,” alisema Rais wa zamani wa Ethiopia Salhe-Work Zewde baada ya mkutano wake na Rais Tshisekedi, ambaye, kwa upande wake, alikaribisha mpango huo wakati wa kikao cha kazi.

Ziara ya kwanza ya jopo la AU kwenda Kigali

Ujumbe wa tathmini wa AU, ulioanzia nchini DRC, unatarajiwa kuendelea leo Ijumaa, Januari 30, kwa mkutano na Rais wa Rwanda Paul Kagame huko Kigali. Hii inaashiria safari ya kwanza ya kundi la ujumbe huo kwenda mji mkuu wa Rwanda, wiki chache tu baada ya mkutano wa kuratibu michakato ya amani kwa mashariki mwa DRC, uliofanyika Togo katikati ya mwezi Januari. Katika Lomé, washiriki walikubaliana kuhusu hitaji la kuimarisha upatanishi wa Kiafrika: “AU lazima ichukue jukumu muhimu” katika utekelezaji wa michakato ya Washington na Doha, Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda Olivier Nduhungirehe alisema, anaripoti mwandishi wetu nchini Rwanda, Lucie Mouillaud.

Ingawa baadhi ya wajumbe wa jopo hilo walitembelea Rwanda mwaka jana—hasa Rais wa zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo, ambaye alikuwa na jukumu la masuala ya ulinzi na usalama ndani ya timu ya upatanishi—wengine bado hawajafanya ziara rasmi Kigali tangu walipochukua nafasi zao ndani ya juhudi za uwezeshaji zinazoongozwa na AU. Hivi ndivyo ilivyo kwa Catherine Samba-Panza, ais wa zamani wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na Sahle-Work Zewde, rais wa zamani wa Ethiopia, miongoni mwa wengine.

Baada ya Rwanda, wawezeshaji wa AU wanatarajiwa mjini Gitega, Burundi, kwa mkutano wa awali na nchi hiyo ambayo inatarajiwa kuchukua uenyekiti wa Umoja wa Afrika mwezi ujao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *