Papa Leo ametoa wito wa mazungumzo ya “dhati na yenye ufanisi” ili kuzuia machafuko na mateso zaidi kwa wananchi wa Cuba.
Akizungumza baada ya sala yake ya kila wiki mjini Vatican, Papa Leo amesema amepokea taarifa za kutia hofu kuhusu hali hiyo, na akaungana na maaskofu wa Cuba kuhimiza viongozi husika kuchagua njia ya mazungumzo badala ya mgogoro.
Mvutano umeongezeka baada ya Rais Donald Trump kutangaza ushuru kwa bidhaa kutoka nchi zinazoiuzia Cuba mafuta, hatua inayolenga kuongeza shinikizo kwa watawala mjini Havana baada ya kumwondoa madarakani mshirika wao wa muda mrefu, Rais Nicolás Maduro wa Venezuela, mapema Januari.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba, Bruno Rodriguez, ametangaza hali ya dharura ya kimataifa, akisema hatua ya Marekani kama tishio kubwa na lisilo la kawaida. Hata hivyo, Trump amesisitiza kuwa Marekani imeanza mazungumzo na viongozi wa Cuba, akisema mgogoro huo haupaswi kugeuka kuwa janga la kibinadamu.
