
Yanga itaanza kutetea taji lake la Shirikisho la CRDB kwa kukabiliana na Cosmopolitan wiki ijayo kwenye Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam.
Mchezo huo ni wa hatua ya 64 bora ya mashindano hayo ambayo bingwa wake anapata tiketi ya kuiwakilisha Tanzania katika Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika droo ya hatua hiyo iliyofanyika Dar es Salaam leo, mabingwa mara tatu wa mashindano hayo, Simba wamepangwa kukutana na Greenland FC ya Kagera.
Azam FC ambayo ilitwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika mwaka 2019 nayo itaanzia nyumbani kwa kuikaribisha Endument ya Kilimanjaro.
Wana fainali wa msimu uliopita, Singida Black Stars nao wataanzia nyumbani kwa kucheza na Copco ya Mwanza wakati huo KMC ikipangwa kucheza na Bandari Tanzania.
Kutakuwa na mchezo wa watani wa jadi wa mkoa wa Tabora ambao utazikutanisha TRA United na Rhino Rangers na mwingine wa mkoa wa Dar es Salaam baina ya JKT Tanzania na Pan African.
Mabingwa wa zamani wa mashindano hayo, Mtibwa Sugar watacheza na IAA na Coastal Union wataikaribisha Nyumbu FC.
Ofisa Mashindano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto amesema kuwa mechi hizo zitachezwa wiki ijayo.
“Kuna baadhi ya viwanja vinatumika na timu zaidi ya moja kwa hiyo lazima zipeane nafasi lakini hatua ya 64 bora itachezwa kuanzia tarehe 17 Februari hadi tarehe 19 Februari,” amesema Kizuguto.
Mechi za 64 Bora Kombe la Shirikisho la CRDB
Mbeya Kwanza vs FGA Talent
Kagera Sugar vs Mighty Elephant
Geita Gold vs Kajuna
Kengold vs Magereza FC
B19FC vs Dhujau
Mbuni vs The Green FC
Transit Camp vs Chama la Wana
Barberian vs Kijiwe Nongwa
Songea United vs Vijana FC
Gunners FC vs Airport FC
Bigman vs Nyika
TMA vs Newala FC
Polisi Tanzania vs THB
Hausung vs West Singers
Stand United vs Mabao
African Sports vs Kilimo FC
Tanzania Prisons vs Moro Kids
Mbeya City vs Biashara United
Coastal Union vs Nyumbu FC
TRA United vs Rhino Rangers
Simba vs Greenland FC
JKT Tanzania vs Pan African
Mtibwa Sugar vs IAA
Fountain Gate vs Mapinduzi
Namungo FC vs Magnet FC
Pamba Jiji vs Alliance
Dodoma Jiji vs Kilimanjaro Wonders
Yanga vs Cosmopolitan
Azam FC vs Endument FC
Singida Black Stars vs Copco
KMC vs Bandari Tanzania
Mashujaa vs Nkim FC