Dar es Salaam. Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waibua shangwe baada ya mwenyekiti wao, Tundu Lissu kupandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu, Dar es Salaam ambapo kesi ya uhaini inayomkabili inatarajiwa kuendelea kuunguruma leo, Februari 9, 2026.

Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka utajibu hoja za kisheria za pingamizi la Lissu kuhusiana na uhalali wa mashahidi fiche wa Jamhuri.

Lissu alivyopandishwa kizimbani Mahakama Kuu

Kesi imepangwa kuanza tena leo kwa siku 20 mfululizo za kazi, mpaka Machi 6, 2026.

Lissu anakabiliwa na shtaka la uhaini, kinyume na kifungu cha 39(2)(d) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, linalotokana na maneno aliyoyatamka kuhusiana na kuzuia kufanyika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Kesi hiyo inayosikilizwa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam na jopo la majaji watatu linaloongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Iringa, Dunstan Ndunguru, akishirikiana na majaji James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde, iko katika hatua ya usikilizwaji wa ushahidi wa upande wa mashtaka.

Mara ya mwisho kesi hiyo iliahirishwa Novemba 12, 2025 baada ya kumalizika kwa kikao (session) cha usikilizwaji wa kesi hiyo kilichoanza Septemba 8, 2025, ambapo mashahidi watatu wa Jamhuri, wote wakiwa ni maofisa wa Polisi, walitoa ushahidi wao.

Endelea kufuatilia Mwananchi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *