.

Chanzo cha picha, Reuters

Waziri Mkuu
wa Israeli Benjamin Netanyahu amesema siku ya Jumapili kwamba alimwambia Rais
wa Marekani Donald Trump wiki iliyopita kuwa makubaliano yoyote ya Marekani na Iran lazima
yajumuishe kuharibiwa kwa miundombinu ya nyuklia ya Iran, si tu kusimamisha
mchakato wa urutubishaji.

Akizungumza
katika Mkutano wa kila mwaka wa Marais wa Mashirika Makuu ya Kiyahudi ya
Marekani, Netanyahu pia alisema Israeli bado inahitaji “kukamilisha
kazi” ya kuharibu handaki zote huko Gaza. Israel, ilisema, tayari imebomoa
kilomita 150 (maili 93) za takriban kilomita 500.

Duru ya pili
ya mazungumzo kati ya Marekani na Iran imepangwa kufanyika wiki hii. Iran
inafuatilia makubaliano ya nyuklia na Marekani ambayo yatafaida pande zote
mbili kiuchumi, mwanadiplomasia wa Iran aliripotiwa kusema Jumapili.

Netanyahu
alisema ana mashaka kuhusu makubaliano lakini lazima yajumuishe kuondolewa kwa nyenzo
zilizorutubishwa nchini Iran. “Hakutakuwa na uwezo wa urutubishaji – sio
kusimamisha mchakato huo, lakini kuharibu vifaa na miundombinu inayowezesha
urutubishaji,” alisema.

Iran na
Marekani zilianzisha upya mazungumzo mapema mwezi huu ili kushughulikia mzozo
wao wa miongo kadhaa kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran na kuepusha mzozo mpya
wa kijeshi.

Marekani
imetuma meli ya pili ya kivita katika eneo hilo na inajiandaa kwa uwezekano wa operesheni
ya kijeshi ikiwa mazungumzo hayo hayatafanikiwa, maafisa wa Marekani wameiambia
Reuters.

Soma zaidi:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *