Darasa katika mji wa Havana, Cuba, ambapo wanafunzi wenye sare nyeupe na nyekundu wanajifunza Kiswahili, na mwalimu akiwasilisha kwenye skrini.

Ili kufahamu zaidi kuhusu hatua hii na mafanikio yaliyofikiwa hadi kufikia sasa, Anold Kayanda wa Idhaa ya Umoja wa Mataifa amemtembelea Profesa Barbara Batte, Mkufunzi anayefundisha lugha ya Kiswahili, yeye na wenzake katika Chuo Kikuu cha Havana na katika Nyumba ya Afrika nchini Cuba.

Kikundi cha wanafunzi wadogo na mtu mzima wameketi pamoja kwenye benchi la jiwe huko Havana, Cuba, wakifanya shughuli za kujifunza zinazohusiana na elimu ya lugha ya Kiswahili.

Takribani miaka 43 iliyopita, Barbara Batte Guevara, alijifunza kwa muda mfupi lugha ya Kiswahili nchini Tanzania lakini mbegu hiyo iliyopandwa karibia nusu karne iliyopita, anataka aipande kwa Wacuba wengine ili ichipue na kuzaa miche zaidi ya lugha ya Kiswahili kote Cuba, ukanda wa Karibiani na hata kote Amerika.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *