Rais wa Marekani Donald Trump anakataa kukubali kushindwa, lakini uamuzi huu wa Mahakama Kuu unahatarisha kuzua migawanyiko zaidi ndani ya Chama cha Republican, kwani baadhi ya maafisa waliochaguliwa hawaungi mkono sera za biashara za Donald Trump, anaripoti mwandishi wetu huko New York, Loubna Anaki. 

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Kwa mtazamo wa kisheria na kikatiba pekee, mamlaka ya kutoza ushuru inabaki kwa Bunge, jambo ambalo lilithibitishwa tena na Mahakama Kuu siku ya Ijumaa.

Kama viongozi walio wengi wa Republican katika Baraza la Seneti na Baraza la Wawakilishi wote wakisisitiza ufanisi wa ushuru uliowekwa na Donald Trump, hakuna aliyetoa maoni kuhusu uwezekano wa kuurejesha au kumpa rais mamlaka ya kuutoza tena. Wanajua kwamba suala hilo linaleta mgawanyiko ndani ya chama chao. Hata hivyo, hivi majuzi, baadhi ya maafisa waliochaguliwa wa chama cha Republican walijiunga na maafisa waliochaguliwa kutoka chama cha Democratic katika kutoa wito wa kufutwa kwa ushuru uliowekwa kwa Canada

Kwa hivyo haishangazi kwamba jana, baadhi ya Warepublican, kama Mitch McConnell, walikaribisha waziwazi uamuzi wa Mahakama Kuu. Seneta huyo anabainisha kwamba ikiwa Ikulu ya White House inataka kutoza ushuru ambao utaathiri uwezo wa ununuzi wa Wamarekani, inahitaji tu “kuwashawishi wawakilishi wao,” akimaanisha Bunge.

Labda ni kwa sababu anajua hana uungwaji mkono wa walio wengi kutoka kambi yake ndio maana Donald Trump kwa sasa anaepuka kuomba Bunge limuunge mkono na anapendelea kutumia sheria zingine zinazomruhusu kuweka ushuru wa muda.

Mahakama ya juu zaidi nchini Marekani iliamua siku ya Ijumaa, Februari 20, kwamba Donald Trump alikuwa amezidi mamlaka yake ya kikatiba kwa kuweka, mnamo mwezi Aprili 2025, ushuru unaoitwa “wa pande zote” kwa karibu bidhaa zote zinazoingia nchini. Uamuzi uliopitishwa na majaji sita dhidi ya watatu, ambao rais wa Marekani alijibu mara moja kwa kutaja uamuzi wa “fedheha” na kutangaza kuanzishwa kwa ushuru mpya wa “kimataifa” wa 10%.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *