
Rais Trump alipotangaza kifo cha Kiongozi Mku wa kiroho wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, matukio ya shangwe yalionekana katika baadhi ya vitongoji vya Tehran na katika majimbo mengine, anaripoti mwandishi wetu huko Tehran, Siavosh Ghazi. Na asubuhi ya leo, tangu televisheni ya serikali ilipothibitisha saa 11:00 aalfajiri (saa za Iran) kifo cha Ali Khamenei, umati wa watu umekusanyika mjini Tehran. Watu wanaomboleza, wanalia, wamekasirika sana, na wanaomba kulipiza kisasi.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Baraza la mwongozo litaanzishwa, ikiwa ni pamoja na Rais wa Jamhuri, mkuu wa mahakama, na mjumbe wa kidini wa Baraza la Walinzi, kusimamia mpito. Kisha, kulingana na Katiba, Bunge la Wataalamu, ambalo lina watu wapatao 90 wa kidini, litaamua kuhusu mrithi wa Kiongozi Mkuu wa Iran.
Mchakato wa mpito baada ya kifo cha Khamenei kuanza Jumapili
“Baraza la uongozi wa muda litaundwa hivi karibuni. Rais, mkuu wa mahakama, na mtaalamu wa sheria kutoka Baraza la Walinzi watachukua jukumu hadi uchaguzi wa kiongozi ajaye,” amesema afisa mkuu wa usalama wa nchi hiyo, Ali Larijani, mkuu wa chombo cha juu zaidi cha usalama cha Iran, Baraza Kuu la Usalama wa Kitaifa, na mshauri wa zamani wa Ali Khamenei. “Baraza hili litaanzishwa haraka iwezekanavyo. Tunafanya kazi ya kuunda kwake kuanzia leo,” ameongeza.
Mfululizo mpya wa milipuko wasikika Dubai
Waandishi wa habari wa AFP huko Dubai walisikia mfululizo wa pili wa milipuko leo Jumapili asubuhi, siku moja baada ya Iran kuanza mashambulizi yake katika Ghuba kulipiza kisasi kwa mashambulizi ya Marekani na Israel yaliyomuua kiongozi mkuu wa Iran.