Wakishutumiwa na mamlaka kwa kukusanya fedha haramu na utakatishaji fedha, angalau wanachama saba wa mpango uliozinduliwa mwaka jana ili kuvunja kizuizi cha Israel dhidi ya eneo la Wapalestina walikamatwa mwishoni mwa wiki iliyopita katika eneo la Sidi Bou Said. Global Sumud Flotilla, ambayo inalaani kukamatwa kwao kama “kiholela,” inadai kuachiliwa kwao mara moja.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Nchini Tunisia, angalau wanachama saba wa Global Sumud Flotilla (GSF), iliyozinduliwa mwaka jana na mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali ili kuvunja kizuizi cha baharini kilichowekwa na Israel kwenye Ukanda wa Gaza, walikamatwa mwishoni mwa wiki iliyopita na kikosi cha kupambana na ugaidi katika eneo la Sidi Bou Said. Mamlaka inawashutumu kwa kukusanya na kufuja fedha kinyume cha sheria wakati wa maandalizi ya msafara wa kundi la kwanza kuelekea eneo la Palestina mwezi Septemba mwaka uliyopita.

GSF, ambayo inakataa tuhuma hizi, inadai kuachiliwa mara moja kwa wanachama wake saba ambao walitarajiwa kufika mbele ya jaji mwishoni mwa wiki na ambao kuzuiliwa kwao kuliongezwa kwa siku tano Jumatano, Machi 11. “Watu hawa walikamatwa kiholela: ripoti [yetu] ya kifedha imechapishwa nchini Tunisia kwa miezi mitatu. Wanachama wetu wangeweza kuhojiwa bila kukamatwa,” anasema Aziz Rhali, mfamasia, raia wa Morocco na mjumbe wa kamati ya uratibu ya GSF. Hata hivyo, anafafanua kwamba licha ya tukio hili, kuondoka kwa meli inayofuata kwenda Gaza, iliyopangwa kwa siku za usoni, bado kunaendelea.

“Tunisia inatumia njia hizi kudhoofisha shughuli zote za Global Sumud Flotilla,” amesema Aziz Rhali, mjumbe wa kamati ya uratibu ya Global Sumud Flotilla.

Katika taarifa, GSF pia inaelezea wasiwasi kuhusu kile inachokiona kama “kuvunjika” katika utamaduni mrefu wa Tunisia wa mshikamano kwa kadhi ya Palestina.

Meli ya kwanza ya shirika hilo, iliyoondoka bandari ya Sidi Bou Said kuelekea Gaza mwezi Septemba mwaka uliyopita, ilikuwa wakati wa kihistoria kwao, licha ya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani yaliyolenga meli zao mbili. Baada ya kuarifiwa, mamlaka ya Tunisia ililaani “uchokozi uliopangwa mapema.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *