
Jeshi la Iran limeonya nchi katika eneo hilo dhidi ya ushirikiano wowote na kituo cha televisheni cha Iran International chenye makao yake makuu London, nchini Uingereza, likisema kwamba miundombinu inayotumika kuunga mkono kituo hicho italengwa kwa mashambulizi.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
“Kwa kutumia uwezo wa setilaiti na miundombinu ya vyombo vya habari vya baadhi ya katika eneo hilo,” kituo hicho cha televisheni “kinarusha vipindi vyake kuchochea vurugu na mvutano, kutengeneza habari za uongo (…) ili kutimiza malengo ya mhalifu Marekani na utawala wa Kizayuni,” kamandi ya jeshi la Iran ya Khatam al-Anbiya imesema katika taarifa iliyotolewa Jumapili jioni, huku ikitishia “kuorodhesha” “nchi au mtu yeye yote atakaye kuwa na ushirikiano” na “kituo hiki kiovu” kuwa katika “malengo ya ya mashambulizi ya Jamhuri ya Kiislamu.”
Mahali inayopatikana miundombinu inayotumiwa na kituo cha televisheni cha Iran International katika eneo hilo hapajulikani kwa sasa.
Iran imeainisha Iran International kama “kundi la kigaidi” tangu mwaka 2022, na katika miezi ya hivi karibuni imesema kwamba kituo hicho kiina uhusiano na Israel, ikionya kwamba ushirikiano wowote na Iran International utawekewa vikwazo.