
Nchini Gabon, uamuzi wa mahakama ya mwanzo ya Libreville ulitarajiwa sana jana, Jumatatu, Machi 16. Chama cha upinzani, Ensemble pour le Gabon (Together for Gabon), kinachoongozwa na Alain-Claude Bilie-By-Nze—kiongozi maarufu wa upinzani—kiliwasilisha malalamiko katika mahakama ya Libreville dhidi ya Mamlaka Kuu ya Mawasiliano (HAC), ambayo ilizima mitandao ya kijamii nchini mwezi mmoja uliopita.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Chama cha Ensemble pour le Gabon kinaishutumu Mamlaka Kuu ya Mawasiliano (HAC) kwa “matumizi mabaya ya madaraka” na ukiukaji wa uhuru wa msingi. Kesi ya awali ilisikika wiki iliyopita. Jana, Jumatatu, uamuzi wa mahakama ulitolewa: ilitangaza kuwa haina uwezo, anaripoti mwandishi wetu huko Libreville, Yves-Laurent Goma.
Ushindi kwa HAC
Uamuzi wa mahakama ni ushindi kwa HAC na wakili wake. Wakati kesi hiyo ilisikilizwa wiki iliyopita, Anges-Kevin Nzigou, wakili wa Mamlaka Kuu ya Mawasiliano (HAC), alipinga kuwa mahakama haina uwezo wa kushughulikia kesi hiyo , akisema kwamba mgogoro huo unatakiwa kushughulikiwa na mamlaka ya mahakama ya utawala. Katika kesi hii maalum, mahakama husika ya utawala ni Baraza la Nchi, taasisi iliyoteuliwa na mahakama ya chini kusikiliza kesi hiyo.
Soma piaGabon: Mamlaka yazima mitandao ya kijamii hadi hatu nyingine itakapochukuliwa
Kwa upande wake, Ensemble pour le Gabon, chama cha Alain Claude Bilie-By-Nze, ambacho kiliwasilisha malalamiko hayo, kilisema kwamba hakikuridhika kabisa na uamuzi wa majaji. Kulingana na Sosthène Sarah Ognyane, wakili wa chama hicho, “Uamuzi huu unatia shaka katika mambo mengi. Mahakama ya Katiba inasema ni sheria ya udhibiti inayoandaliwa. Na inapokuwa sheria ya udhibiti ya maandalizi, inamaanisha kwamba si sheria ya utawala wala sheria ya udhibiti. Kwa hivyo, haiwezi kuwasilishwa mbele ya Baraza la Nchi.”
Wengi waamua kutumia VPN
Katika taarifa, chama cha Bilie-By-Nze kilitangaza kukata rufaa. Wakati huo huo, mitandao ya kijamii bado imezimwa. Hata hivyo, watu wengi wameamua kutumia VPN ili kukabiliana na hali hii ya kuzimwa kwa mitandao ya kijamii.