Mnamo Machi 16, 2026, jeshi la Kongo liliwakamata viongozi wawili wa kundi lenye silaha la Wazalendo huko Walikale, mashariki mwa nchi hiyo. Makundi haya yanashirikiana na vikosi vya serikali (FARDC) katika vita dhidi ya waasi wa AFC/M23.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 2 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mara nyingi hujulikana kama Wazalendo, wapiganaji hawa wanaunga mkono FARDC katika vita katika maeneo kadhaa katika sehemu ya mashariki ya nchi. Hata hivyo, wanamgambo hawa pia hushutumiwa mara kwa mara kwa unyanyasaji na uporaji dhidi ya raia na wakati mwingine hushiriki katika vita vya ndani. Uongozi wongozi wa jeshi umeghadhabishwa na kurudia tena kwa mapigano haya kati ya makundi ya Wazalendo.

Wapiganaji wawili waliokamatwa mashariki mwa DRC ni Kirikicho Mirimba, wa kundi la muungano wa Wazalendo nchini Kongo (Copaco), na Musubao Kalimba, maarufu kama “Kasilasi,” linaloendesha harakati zake hasa katika maeneo ya Kalehe, Masisi, na Walikale, katika mikoa ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini.

Kirikicho Mirimba na Musubao Kalimba ni sehemu ya Wazalendo, makundi haya yenye silaha, yanayopigana pamoja na jeshi la Kongo dhidi ya waasi wa AFC/M23 mashariki mwa nchi.

Lakini jeshi linawashutumu kwa kupigana kati yao wenyewe: kwa mwaka mmoja na nusu uliopita, wapiganaji wa Kirikicho na wale wa Musubao wamekuwa wakipigana mara kwa mara. Hizi ni vita kati ya wanamgambo wanaodaiwa kutetea upande mmoja, dhidi ya adui mmoja.

Madhara kwa raia ni makubwa. Kwa mfano, kati ya Februari 15 na 18, katika eneo la uchifu la Buhavu, pia katika eneo la Kalehe, mapigano haya yalisababisha vifo vya raia 14 na wanawake 7 kubakwa. Mali iliporwa. Watu walitoroka makazi yao.

Wawili hao walikamatwa huko Walikale, Kivu Kaskazini. Watalazimika kujibu mbele ya mahakama ya kijeshi.

Historia ndefu ya vurugu

Kirikicho Mirimba anatoka eneo la Ziralo, huko Kalehe. Anaongoza wanamgambo wanaojulikana kama Mai-Mai Kirikicho, wanaoundwa zaidi na watu wa kabila la Tembo. Kundi hili lenye silaha limekuwa likiendesha harakati zake kwa miaka mingi katika misitu ya eneo hili la Kivu Kusini, na pia katika baadhi ya maeneo ya jirani ya Kivu Kaskazini. Jina lake linaonekana katika ripoti kadhaa za Umoja wa Mataifa, haswa kwa kuajiri watoto kama wanajeshi, kuanzia mwaka wa 2009. Kwa miaka kadhaa, ameshutumiwa kwa kudhibiti na kutoza kodi kwenye maeneo ya madini katika eneo hilo, ikiwa ni pamoja na migodi ya dhahabu, cassiterite, na coltan, pamoja na masoko na barabarani.

Hii si mara ya kwanza kwa vitendo vyake kuwa na athari zaidi ya uwanja wa vita. Mnamo mwaka 2018, Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (RSF) lililazimika kupunguza uwepo wake huko Bunyakiri, katika eneo la Kalehe, baada ya mapigano yaliyowahusisha wapiganaji wake. Wakati huoraia wengi waliuawa. Katika miezi ya hivi karibuni, licha ya historia hii mbaya, Kirikicho bado alikuwa mstari wa mbele dhidi ya AFC/M23 huko Kalehe.

Kukamatwa kwake, na kukamatwa kwa Musubao Kalimba, kunakumbusha kwamba mashariki mwa Kongo, vitendo kati ya washirika na wahalifu mara nyingi huwa sawa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *