Mamlaka hiyo ya Urusi katika eneo la Krasnodar, imeripoti kuzuka kwa moto mdogo kwenye kiwanda cha kusafisha mafuta cha Afipski na kusema sehemu za droni moja ziliangukia kiwanda hicho.

Hata hivyo wamesema hakukuwa na majeruhi.

Kulingana na vyanzo Ukraine, kiwanda hicho kinachozalisha petroli na dizeli, awali kilishambuliwa mnamo Agosti 28.

Wataalamu wanakadiria kuwa Urusi imepoteza takriban robo ya uwezo wake wa usindikaji kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya viwanda vya kusafisha mafuta, vituo vya mafuta na vya upakiaji.

Hali hii imesababisha uhaba wa dizeli na petroli katika baadhi ya mikoa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *