Mashambulizi ya ADF, kundi lenye silaha lenye asili ya Uganda lenye uhusiano na Dola la Kiislamu, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, yanaendelea. Mapema mwezi Machi, mashambulizi mawili mfululizo katika eneo la Mambasa la mkoa wa Ituri yalisababisha watu wengi kuhama makazi yao na kukimbilia Bafwasende na hadi Kisangani, katika mkoa jirani wa Tshopo.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Maelfu ya watu wamekimbia vurugu hizo, hasa kutoka Badengaido na vijiji jirani. Raia hao wanalaani ukubwa wa ukatili wa ADF na kuomba hatua kali zaidi kutoka kwa mamlaka.

Sakina alikimbia katikati ya usiku. Katika kijiji cha Muchacha, risasi zilirushwa ghafla, kisha nyumba zikachomwa moto. Baada ya kutembea kilomita kadhaa, alifika Bafwasende. Bado yuko katika hali nzito kutokana na ukubwa wa ukatili wa waasi hao wa Uganda.

“Wakati risasi zilipoanza kurushwa, walianza kuchoma nyumba. Kwa hofu, sote tulikimbia pande tofauti. Tulipokimbia, mtoto wangu alibaki ndani ya nyumba. Watu wengi waliuawa, mali zetu zilichomwa, na mtoto wangu alifariki baada ya nyumba yetu kuchomwa moto. Ninajikuta hapa Bafwasende. Sina chochote nilichonacho,” mwanamke huyo anasimulia.

Shambulio dhidi ya Muchacha lilidaiwa na kundi la Islamic State. Siku chache baadaye, hali kama hiyo ilitokea Badengaido, yapata kilomita kumi kutoka Muchacha.

Watu wengi watoroka makazi yao

TrĂ©sor anakumbuka usiku wa kutisha: milio ya risasi, moto, raia waliolengwa. “Risasi zilirushwa Badengaido. Shule ya kijijini ilichomwa moto, kama vile nyumba ya mkuu wa shule. Tuliona kwamba tishio lilikuwa likizidi kuwa kubwa. Tulikimbia na hapa tuko Bafwasende. Niko hapa na mke wangu na watoto. Kwa kweli, sijui mmoja wa watoto wangu yuko wapi kwa sababu ya kukimbia huku. Tunatafuta na kutumaini kuwa tutampata. Leo, tumekimbia makazi yetu na tuko katika hali mbaya.”

Mashambulizi haya yamesababisha wimbi kubwa la watu waliokimbia makazi yao huko Bafwasende, na hata katika jiji la Kisangani. Katika miezi miwili iliyopita, ADF imekuwa ikihusika na mauaji mengi yaliyofanywa na makundi yyenye silaha, huku karibu raia 100 wakiuawa, pamoja na visa vingi vya utekaji nyara.

Sambamba na vurugu hizo, kundi hilo pia linaweka aina za udhibiti wa kiuchumi: ukusanyaji wa “tokeni” na kodi kwa shughuli za ndani, zilizoanzishwa tangu mwezi Novemba 2025.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *