#MZOZOMAREKANINAIRAN
Marekani imetuma ujumbe kwa Iran kupitia mjumbe maalum, na ujumbe huo uliwasilishwa kwa Iran, kwa mujibu wa shirika la habari la Marekani, CBS News, likinukuu afisa mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran.
Trump alitangaza jana kuwa alikuwa amefanya mazungumzo na Iran kwa muda wa siku mbili, na kwamba mazungumzo hayo yataendelea wiki hii.
Baada ya kauli ya Trump, Iran ilikanusha kuwepo kwa mazungumzo yoyote na Marekani.
Hata hivyo, baadaye Iran ilithibitisha kuwa ujumbe kutoka Marekani uliwasilishwa kupitia nchi nyingine, kama ilivyoripotiwa na CBS News.
“Tumeupokea ujumbe kutoka Marekani. Kwa sasa unafanyiwa tathmini,” alisema afisa mmoja wa Iran, kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari.
Trump alisema katika taarifa yake jana kuwa alikuwa amefanya mazungumzo yenye tija na Iran na kuwasilisha hoja 15.
“Iran inataka amani; ninaamini kuna uwezekano mkubwa wa kufikiwa kwa makubaliano,” Trump aliwaambia waandishi wa habari.
Marekani na Iran hazina uhusiano wa moja kwa moja wa kidiplomasia.
Badala yake, zimekuwa zikiwasiliana na kufanya mazungumzo kupitia nchi nyingine.
#starTvupdate
#chanzobbcswahili

(Feed generated with FetchRSS)