Waziri wa Mambo ya Nje amesema: Iran hadi sasa haijatoa jibu kwa mapendekezo 15 ya Marekani, na wala haijawasilisha sharti lolote.

Sayyid Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, katika mahojiano na televisheni ya Al‑Jazeera, ametoa ufafanuzi kuhusu hali ya sasa ya ubadilishanaji wa ujumbe na Marekani, masharti ya Iran ya kumaliza vita, na pia kuhusu hali ya Lango Bahari la Hormuz.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kinachoendelea “si mazungumzo” bali ni kubadilishana ujumbe; ujumbe ambao hufikishwa moja kwa moja au kupitia “marafiki wa eneo.”

Amesisitiza kuwa bado anapokea ujumbe kutoka Steve Witkoff, mjumbe maalumu wa Marekani, lakini jambo hilo halimaanishi kuwa kuna mazungumzo yanaendelea.

Waziri ameongeza kuwa ujumbe unaobadilishwa kwa kawaida huwa ni “tahadhari au mitazamo ya pande mbili” inayowasilishwa kupitia njia mbalimbali za eneo.

Araghchi amesema hakuna mazungumzo yanayoendelea na upande wowote kwa sura rasmi, na kwamba ujumbe hupitia Wizara ya Mambo ya Nje kwa uratibu kamili na taasisi za kiusalama.

Amebainisha pia kuwa ubadilishanaji wa ujumbe unafanyika katika mfumo rasmi chini ya usimamizi wa serikali na Baraza Kuu la Usalama wa Taifa.

Araghchi amesisitiza kuwa Iran haijatoa jibu kwa mapendekezo 15 ya Marekani kuhusu usitishaji vita, na pia haijawasilisha pendekezo au sharti lolote upande wake.

Amesema Tehran bado haijafanya uamuzi kuhusu asili ya mazungumzo yenyewe, na kwamba masharti ya Iran ya kumaliza vita “yapo wazi kabisa.”

Araghchi amesisitiza tena kuwa Iran “haitakubali kusitisha vita” bila kufikiwa “mwisho kamili wa vita kote katika kanda.”

Masharti aliyoyataja ni “dhamana ya kutokurudiwa kwa mashambulizi” na “kulipwa fidia ya hasara.”

Araghchi amesema “haiwezekani kulitisha taifa la Iran,” na kwamba Rais wa Marekani anapaswa kuwahutu wananchi wa Iran kwa heshima.

Aidha ametangaza kuwa Lango Bahari la Hormuz “liko wazi kikamilifu,” na limefungwa tu kwa wale wanaoshiriki kwenye vita dhidi ya Iran.

Halikadhalika amesema hatua zote muhimu zimechukuliwa ili kuhakikisha meli za mataifa rafiki zinapita bila wasiwasi.

Araghchi ameongeza kuwa Lango Bahari la Hormuz linaweza kuwa “njia ya amani,” na maamuzi juu ya suala hilo yako mikononi mwa nchi zote za pwani za eneo hilo.

Ameonya pia kuwa Iran “iko tayari kwa aina yoyote ya mapambano ya nchi kavu,” huku akibainisha kuwa anataraji maadui “hawatakosoa katika hesabu zao.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *