Kikao cha kusikiliza kesi kilichopangwa kufanyika siku ya Jumatano, Aprili 8, jijini Paris, siku moja baada ya kufunguliwa kwa maadhimisho ya kila mwaka ya mauaji ya kimbari ya Watutsi nchini Rwanda, kimeahirishwa hadi Mei 6.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Mahakama ya Rufaa ya Paris iliomba kuongezwa muda wa majadiliano kuhusu amri ya kuondolewa kwa kesi na kukataliwa kwa hatua za ziada za uchunguzi, ambazo zilimnufaisha Agathe Habyarimana mnamo Agosti 2025. 

Ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma na kundi la vyama vya kiraia kwa ajili ya Rwanda vilikata rufaa kwa uamuzi huu, ambao unalenga kufunga kesi zilizoanzishwa karibu miaka ishirini iliyopita dhidi ya mjane wa rais wa zamani Juvénal Habyarimana.

Ofisi ya mwendesha mashtaka wa umma na vyama vya kiraia vinabaini kwamba vielelezo vingi vilitupiliwa mbali na majaji ambao walihitimisha miezi michache iliyopita kwamba hakukuwa na “ushahidi wa kutosha” dhidi ya Agathe Habyarimana. Amri yao ya kuondolewa kwa kesi hata inamwakilisha mke wa rais wa zamani “si kama mhusika wa mauaji ya kimbari, bali kama mwathirika” wa shambulio baya la ndege ya Juvénal Habyarimana mnamo Aprili 6, 1994, kichocheo cha mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi nchini Rwanda.

“Kesi isiyo na mashiko”?

Wakati upande wa utetezi ukielekeza “kesi isiyo na mashiko” na kutazamiwa kufutwa, upande wa mashtaka na vyama vya kiraia wanabainisha kwamba Agathe Habyarimana alishiriki kikamilifu katika kupanga na kutekeleza mauaji ya kimbari. Kulingana na vyama vya waathiriwa, mke wa rais wa zamani alikuwa mmoja wa viongozi wa “Akazu,” kundi dogo lenye nguvu la Wahutu lililokuwa na mamlaka kubwa nchini Rwanda wakati huo—ambalo uwepo wake unatiliwa shaka na amri ya kufutwa kwa mashitaka.

Ushahidi wawekwa kando

Uhusiano kati ya Agathe Habyarimana na mamluki wa Ufaransa Paul Barril kabla na wakati wa mauaji ya kimbari ya Watutsi havikutajwa na mahakimu – ambao ofisi ya mwendesha mashtaka wa kitaifa wa kupambana na ugaidi inawashutumu kwa kuwatenga mashahidi kadhaa muhimu katika kesi hii.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *