s

Chanzo cha picha, Getty Images

Marekani na Iran zimeshindwa kufikia makubaliano ya kumaliza vita baada ya mazungumzo ya ngazi ya juu yaliyofanyika Islamabad, Pakistan.

Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, amesema licha ya mazungumzo marefu yaliyodumu kwa saa 21, pande hizo mbili hazikuweza kukubaliana juu ya masharti ya mwisho.

Amesema Iran “haikukubali masharti ya Marekani”, huku akisisitiza kuwa Washington inahitaji kuona dhamira ya wazi kutoka Tehran ya kuacha kabisa mpango wa kutengeneza silaha za nyuklia.

Kwa upande wake, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesema mazungumzo hayo yalikuwa “ya kina”, lakini ikaishutumu Marekani kwa kutoa “matakwa makubwa na yasiyo halali”.

Mazungumzo hayo yalikuwa yakisimamiwa na Pakistan, huku Waziri Mkuu wake, Shehbaz Sharif akitajwa kupongezwa kwa juhudi za upatanishi.

Licha ya kushindwa kufikia makubaliano, Donald Trump amesema matokeo hayo “hayajaleta tofauti” kwa Marekani, akisisitiza kuwa nchi yake bado ipo katika nafasi ya ushindi.

Mazungumzo hayo yalikuwa yakilenga kufikia makubaliano ya kusitisha vita vinavyoendelea huko Mashariki ya Kati, lakini hadi sasa hatma ya mgogoro huo bado haijulikani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *