Mashahidi wanasema mamia ya maelfu ya raia bado wamekwama, huku mamlaka za afya zikishindwa kujibu maombi ya uokozi. Jeshi la Israel limesema limeshambulia maeneo 140 ya kijeshi katika saa 24 zilizopita, ambapo watu 21 wameuawa.

Wakati huo huo maandamano makubwa yamefanyika katika miji mbalimbali ya Israel, ikiwemo Tel Aviv na Jerusalem, wanakoendelea kuweka kambi karibu na makaazi ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu, wakishinikiza kukomeshwa kwa operesheni ya Gaza na kuachiwa kwa mateka.

“Familia za mateka zinaomba makubaliano na pia dunia nzima imechoshwa na vita. Hata Waisraeli pia wamechoshwa na vita. Kwa hiyo watu wanataka kuona hili likiisha. Na nafikiri njia pekee ya kumaliza ni kufikia makubaliano yatakayohakikisha usalama, yatakayohakikisha mustakabali bora kwa kila mtu. Na zaidi ya yote yatakayowarejesha nyumbani mateka wetu.”

Mashirika ya afya ya kimataifa yameonya hali ya kibinadamu inazidi kuzorota, huku hospitali kadhaa zikifungwa na mamia ya maelfu ya watu wakiendelea kuikimbia Gaza City.

Shirika la Chakula Duniani linakadiria kuwa hadi watu 400,000 wamekimbia Gaza City, lakini maelfu wengine bado wamekwama kwenye jiji hilo linalozingirwa.
 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *