Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Marco Rubio, amesema hakuna mamlaka yoyote ya Marekani iliyowaambia wanamichezo wa Iran kuwa hawaruhusiwi kushiriki mashindano ya kombe la dunia FIFA yatakayofanyika nchini humo msimu huu wa joto.

Amesema kumekuwa na uvumi kuwa Iran huenda isishiriki na kwamba Italia inaweza kuchukua nafasi yao, lakini akaongeza kuwa ikiwa Iran haitashiriki, huo utakuwa uamuzi wao wenyewe.

Rubio alieleza kuwa tatizo si wanamichezo wa Iran, bali ni baadhi ya watu wanaoweza kuandamana nao.

“Wasichoweza kufanya ni kuingiza magaidi wa IRGC nchini kwetu na kujifanya waandishi wa habari au wakufunzi wa michezo,” alisema.

#Chanzobbcswahili

(Feed generated with FetchRSS)

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *