Serikali ya Côte d’Ivoire imevunja Tume Huru ya Uchaguzi (CEI) siku ya Jumatano, Mei 6, kufuatia ukosoaji mwingi dhidi ya chombo hicho. Mfumo mpya wa usimamizi wa uchaguzi unatarajiwa kuwekwa hivi karibuni, kulingana na msemaji wa serikali.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Serikali ya Côte d’Ivoire imvunja Tume Huru ya Uchaguzi (CEI) siku ya Jumatano, Mei 6, 2026, wakati wa mkutano wa baraza la mawaziri uliofanyika katika Ikulu ya rais chini ya ukiongozwa na rais Alassane Ouattara.

Kulingana na msemaji wa serikali Amadou Coulibaly, baraza la mawaziri lilipitisha, chini ya mamlaka ya Wizara ya Mambo ya Ndani na Usalama, amri ya kufuta taasisi hiyo.

Uamuzi huu unakuja mwishoni mwa mzunguko uliopita wa uchaguzi. Serikali inahalalisha kuvunjwa kwa CEI kutokana na wasiwasi uliotolewa kuhusu taasisi hiyo na ukosoaji unaorudiwa ambao imekabiliana nao kwa miaka mingi.

Kulingana na mamlaka, mapungufu haya yalisababisha kuzingatiwa kwa mageuzi ya kina ya mfumo wa uchaguzi. Kuvunjwa kwa Tume Huru ya Uchaguzi (IEC) kunalenga kufungua njia ya kuanzishwa kwa utaratibu mpya wa usimamizi wa uchaguzi, ambao unaweza kuimarisha imani ya wadau wa kisiasa na raia.

Tume Huru ya Uchaguzi iliyoanzishwa na Sheria Nambari 2001-634 ya Oktoba 9, 2001, kwa mujibu wa Katiba ya Agosti 1, 2000, ilikuwa imepewa jukumu la kuandaa na kusimamia uchaguzi katika ngazi ya kitaifa na kura za maoni nchini Côte d’Ivoire kwa karibu miaka 25.

Serikali iinakusudia, kupitia mageuzi haya, kuhakikisha kunafanyika uchaguzi wa amani, wa uwazi na wa kuaminika nchini Côte d’Ivoire.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *