H

Chanzo cha picha, CGTN

Rais wa China Xi Jinping ametoa wito kwa nchi yake na Marekani kushirikiana kama washirika badala ya kuwa wapinzani, akisisitiza haja ya utulivu katika uhusiano wa mataifa hayo mawili yenye ushawishi mkubwa duniani.

Akizungumza katika hotuba ya ufunguzi, Xi amesema dunia nzima inafuatilia mazungumzo yao, akibainisha kuwa mabadiliko makubwa ya kimataifa yasiyo ya kawaida yanaendelea kwa kasi na hali ya kimataifa iko katika mzunguko wa mabadiliko na misukosuko.

Aliongeza kuwa dunia imefika katika njia panda mpya, akihoji iwapo China na Marekani zinaweza kuepuka kile kinachoitwa “mtego wa Thucydides” na badala yake kuanzisha mfumo mpya wa mahusiano unaoweza kuleta utulivu wa kimataifa.

Xi amehoji pia iwapo mataifa hayo mawili yanaweza kushirikiana kukabiliana na changamoto za dunia na kujenga mustakabali bora wa mahusiano yao kwa maslahi ya watu wao na binadamu kwa ujumla.

Pia amewapongeza Marekani na Rais Donald Trump kwa kuadhimisha miaka 250 ya uhuru, akisema nchi hizo mbili zina maslahi mengi yanayofanana kuliko tofauti.

Amesisitiza kuwa mafanikio ya upande mmoja yanaweza kuwa fursa kwa mwingine, na kwamba uhusiano thabiti kati ya China na Marekani ni muhimu kwa utulivu wa dunia.

“China na Marekani zinanufaika na ushirikiano na hupoteza kupitia migogoro,” amesema, akihitimisha kwa wito wa mataifa hayo kuwa washirika na kusaidiana kufanikiwa katika enzi mpya ya mahusiano ya kimataifa.

Soma zaidi:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *