Chanzo cha picha, Getty Images
Rais wa Marekani Donald Trump, amesema kuwa ameagiza kusitishwa kwa shambulio jipya la kijeshi dhidi ya Iran kwa ombi la viongozi wa mataifa ya Kiarabu ya eneo hilo, akiongezea kuwa mazungumzo na Tehran karibu yanaafikia makubaliano ambayo yataizuia Iran kumiliki silaha za nyuklia.
Trump alisema kuwa amesitisha operesheni za kijeshi kwa siku mbili au tatu ili kutoa nafasi kwa mazungumzo hayo kufanyika pamoja na mashauriano na viongozi wa eneo kutoka Saudi Arabia, Falme za Kiarabu na Qatar.
Iran pamoja na mataifa hayo ya Kiarabu hazijajibu matamshi ya Trump, lakini makao makuu ya jeshi la Iran mjini Tehran yalisema vikosi vya kijeshi vya nchi hiyo “vina nguvu zaidi na vimejiandaa zaidi kuliko hapo awali.”
Pia unaweza kusoma:
