
Ingawa matokeo ya mwisho ya duru ya pili ya uchaguzi wa wabunge bado hayajatangazwa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, mkuu wa nchi ametangaza muundo wa serikali yake mpya siku ya Alhamisi, Mei 21. Ikiwa na wajumbe 29, inajumuisha mawaziri wapya 10 pekee.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, mwezi mmoja baada ya kuapishwa kwake kwa muhula wa tatu, Rais Faustin-Archange Touadéra aliteua serikali mpya, ofisi ya rais ilitangazwa siku ya Alhamisi, Mei 21. Mkuu wa nchi tangu mwaka 2016, Faustin-Archange Touadéra alichaguliwa tena mwezi Desemba kwa asilimia 77.90 ya kura katika uchaguzi uliopingwa na upinzani, hasa na mpinzani wake mkuu, Anicet-Georges Dologuélé, ambaye alilaani “udanganyifu mkubwa.”
Waziri Mkuu Félix Moloua, ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2022, aliwasilisha barua ya kujiuzulu kwake Mei 13, kabla ya kuteuliwa tena siku mbili baadaye na mkuu wa nchi. Ni mawaziri wapya 10 pekee ambao wamejiunga na serikali hii yenye wajumbe 29, kulingana na taarifa iliyotolewa naofisi ya rais. Serikali hiyo inatawaliwa na watu walio karibu na chama cha United Hearts (MCU), chama cha rais. Miongoni mwa walioteuliwa wapya, Evariste Ngamana anakuwa Waziri wa Mawasiliano na Vyombo vya Habari. Alikuwa msemaji wa Faustin-Archange Touadéra wakati wa kampeni za uchaguzi uliopita.
Upinzani mara kwa mara unashutumu mkuu wa nchi kujipa madaraka makubwa na unaomba mazungumzo makubwa ya kitaifa. Uteuzi wa serikali hii mpya unafuatia ufunguzi wa bunge la nane mwanzoni mwa mwezi Mei, ingawa matokeo ya mwisho ya duru ya pili ya uchaguzi wa wabunge bado yanasubiriwa. Ni wabunge 90 pekee ambao wameapishwa rasmi katika Bunge la taifa lenye viti 144. Viti 54 vilivyobaki vinatarajiwa kujazwa mara tu matokeo yatakapotangazwa na, kwa baadhi, baada ya uchaguzi wa sehemu.
