JD Vance: Marekani na Iran ‘zakaribia’ kufikia makubaliano, lakini mazungumzo bado hayajakamilikaJD Vance: Marekani na Iran ‘zakaribia’ kufikia makubaliano, lakini mazungumzo bado hayajakamilika

n

Chanzo cha picha, AFP

Katibu Mkuu wa Chama cha Madaktari, Wafamasia na Madaktari wa Meno nchini Kenya (KMPDU), Davji Bhimji Atellah, amehoji sababu za Kenya kuripotiwa kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa kito cha karantini na matibabu ya Ebola kwa watu waliokumbana na virusi hivyo, katika Kituo cha Jeshi la Anga cha Laikipia.

Katika taarifa iliyotolewa Mei 28, Atellah alieleza hasira yake kuhusu mpango huo na kuishutumu serikali kwa kile alichosema ni kuweka maslahi ya mataifa ya kigeni mbele ya usalama wa raia wa Kenya.

“Kama walinzi wakuu wa mfumo wa afya wa Kenya, tunasikitishwa sana na utayari unaoonekana wa serikali kuhatarisha usalama wa kibaolojia wa taifa na maisha ya wananchi wake kwa ajili ya misaada ya kigeni,” chama hicho kilisema.

KMPDU sasa inamtaka Waziri wa Afya, Aden Duale, pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje kueleza kwa nini Kenya ilichaguliwa badala ya nchi zilizo karibu zaidi na kitovu cha mlipuko wa Ebola.

“Hatutakaa kimya tukitazama Kenya ikigeuzwa kuwa eneo la kudhibiti ugonjwa hatari ambao hatukuusababisha,” aliongeza.

Atellah alisema kuwa katika milipuko iliyopita, Marekani ilikuwa ikipeleka raia wake nyumbani kwa matibabu badala ya kuwahamishia nchi nyingine.

KMPDU pia imetaka makubaliano yoyote ya ushirikiano kati ya Kenya na Marekani kuhusu mpango huo kuwekwa wazi mara moja.

Kauli zake zimekuja wakati mjadala mkubwa ukiendelea nchini Kenya kufuatia taarifa kuwa Marekani huenda ikawapeleka watu waliokumbana na Ebola nchini Kenya kwa uchunguzi au matibabu.

Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Huduma za Matibabu, Ouma Oluga, amesema ushiriki wa Kenya katika kukabiliana na majanga ya afya duniani si suala la kuhatarisha taifa bali ni wajibu wa kitaalamu unaotokana na uzoefu wa nchi hiyo.

“Huu ni wakati wa Kenya kujitokeza,” alisema, akiongeza kuwa mchango wa Kenya katika kudhibiti milipuko ya magonjwa katika ukanda na duniani unaonyesha uzoefu mkubwa wa muda mrefu katika usimamizi wa dharura za afya ya umma.

Wizara ya Afya imesisitiza kuwa hatua za Kenya zitaendelea kuongozwa na sayansi, mifumo ya kisheria na masharti madhubuti ya afya ya umma huku ikijaribu kusawazisha ushirikiano wa kimataifa na usalama wa wananchi wa ndani.

Soma zaidi:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *