
Mapigano kati ya Iran na Israel yamesitishwa siku ya Jumatatu, Juni 8, baada ya mashambulizi ya pande zote kwa mara ya kwanza tangu makubaliano ya kusitisha mapigano yalipofikiwa miezi miwili iliyopita.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Siku ya Jumatatu, Juni 8, Iran imetangaza “kukomesha operesheni” dhidi ya Israel, ambayo ililenga “kutoa majibu makali” baada ya mashamulizi ya mabomu katika vitongoji vya kusini mwa Beirut. Hata hivyo, Tehran ilitishia kulipiza kisasi zaidi iwapo mashambulizi zaidi ya Israel yatatokea nchini Lebanon.
Hata hivyo, mashambulizi ya Israel yaliendelea kusini mwa Lebanon dhidi ya maeneo kama kumi na tano, ikiwa ni pamoja na jiji la Tyre, na kuua watu 14 na kujeruhi zaidi ya 20, kulingana na serikali na Shirika la Msalaba Mwekundu. Hezbollah ilidai kuhusika kwa mashambulizi mapya dhidi ya vikosi vya Israel katika eneo la kusini, lakini si katika ardhi ya Israel.
Iran ilirusha makombora ya balestiki kuelekea Israel siku ya Jumapili, Juni 7, ili kulipiza kisasi kwa mashambulizi ya mara kwa mara ya mabomu ya Israel kusini mwa Lebanon na vitongoji vya Beirut. Jeshi la Israel lilisema lilizuia makombora kadhaa. Kwa kujibu, jeshi la Israel lilishambulia malengo ya kijeshi magharibi na katikati mwa Iran usiku wa Juni 7 kuamkia Jumatatu Juni 8. Milipuko ilisikika Tehran, Tabriz, na Isfahan.