Nchini Afrika Kusini, mzozo mpya kati ya balozi wa Marekani na Wizara ya Mambo ya Nje umejitokeza tena. Leo Brent Bozell III, ambaye aliwasili nchini Afrika Kusini mwaka huu, anaikosoa Pretoria kwa kuonyesha urafiki wake kupita kiasi kwa nchi mbili za BRICS, China na Iran, wakati ambapo Washington inashiriki katika mazungumzo na Tehran ili kukomesha vita.

Imechapishwa:

Dakika 1 Wakati wa kusoma

Matangazo ya kibiashara

Na mwandishi wetu huko Johannesburg, Claire Bargelès

Wiki hii, makamu wa rais wa Afrika Kusini alikuwa Beijing, huku naibu waziri wa mahusiano ya kimataifa wa Iran akipokelewa Afrika Kusini. Hili liliudhi ubalozi wa Marekani, ambao ulitoa maoni kwenye mtandao wa kijamii wa X: “Pretoria inalita hili ‘kutofungamana’. Tunazungumzia kile ambacho ni kweli kabisa: chaguo. “

Kwa kujibu, ofisi ya waziri wa mambo ya nje wa Afrika Kusini ilijibu haraka kwamba “kutofungamana hakupaswi kuchanganywa na kutopendelea upande wowote.” Pretoria ilifutlia mbali tena wito wa “kuvutiwa na ushindani wa kijiografia au kushinikizwa kuchukua upande,” ikihifadhi haki ya kukuza uhusiano wa pande mbili na yeyote inayemwona anafaa.

Leo Brent Bozell III alikuwa tayari amekwazana na mamlaka ya Afrika Kusini mapema mwaka huu, kwani aliitwa muda mfupi baada ya kuwasili nchini Afrika Kusini na kuanza kazi yake kwa ukosoaji wake wa mfumo wa sheria au sera unaolenga kurekebisha ukosefu wa usawa wa kijamii. Haya yote yalitokea dhidi ya mashambulizi ya mara kwa mara ya Rais Donald Trump dhidi ya Afrika Kusini kwa uhusiano wake na BRICS, akiishutumu kwa mauaji ya kimbari ya wazungu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *